Wasiojulikana wakwamisha ujenzi hospitali Pangani

Waiba magunia ya misumari

TANGA: Watu wasiojulikana wameiba magunia mawili ya misumari katika mradi wa hospitali ya Wilaya ya Pangani

Mkuu wa Wilaya ya Pangani Zainab Abdallah ameweka bayana hilo wakati wa ziara ya Mwenyekiti wa Chama Cha mapinduzi Mkoa wa Tanga Rajab Abdurahman aliyefanya ziara ya kushtukiza hospitalini hapo.

Amesema kuwa baada ya kubaini wizi huo ameuagiza uongozi wa hospitali hiyo kuweza kuripoti kwenye vyombo husika ili hatua za kisheria ziweze kufuatwa.

“Tayari taarifa imeweza kutolewa na taratibu nyingine zinafuatwa kwani mradi huu ni muhimu kwa wananchi wa Wilaya hii”amesema.

Hata hivyo Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajabu Abdurahman amemuagiza Mkuu wa kituo cha Polisi Wilaya ya Pangani(OCD) kuwachukulia hatua za kisheria wabadhilifu wa vifaa vya ujenzi wa Hospitali ya wilaya hiyo.

Mbali ya agizo hilo pia amemuomba Mkuu wa wilaya hiyo na kamati ya ulinzi na usalama kutembelea mara kwa mara hospitailini hapo  ili kutokuwapa nafasi  watu wanaohujumu mradi huo ambao Serikali imetenga Sh milioni 900 kwa ajili ya maboresho na ujenzi wa majengo mapya.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Wandaeay
Wandaeay
29 days ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 29 days ago by Wandaeay
Back to top button
1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x