WATAHINIWA 613 kati ya 1,136 waliofanya mitihani ya Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi wamefaulu,watahiniwa 48 wamefeli na 474 watarudia mitihani
Akitangaza matokeo ya 25 ya Bodi leo jijini hapa, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo Godfred Mbanyi álisema kuwa mitihani hiyo ilifanyika Novemba 22 hadi 25 mwaka jana nchi nzima .
Álisema kuwa jumla watahiniwa 1,216 walisajiliwa ili kufanya mitihani hiyo, ambapo watahiniwa 1,135 sawa na asilimia 93.
3 walifanya mitihani hiyo.
“Kumekuwepo na ongezeko la watahiniwa ukilinganisha na msimu uliopita uliokuwa na watahiniwa 1,032” álisema
Álisema kuwa kati ya watahiniwa waliofanya mitihani hiyo watahiniwa 452 ni wapya na waliobakia 683 ni watahiniwa waliokuwa wakirudia baadhi ya masomo.
“Jumla ya watahiniwa 613 sawa na asilimia 54 walifaulu mitihani yao,watahiniwa 474 sawa na asilimia 41.8 watarudia baadhi ya masomo kuanzia somo moja hadi masomo matatu kutegemeana na idadi ya masomo aliyofeli na watahiniwa 48 sawa na asilimia 4.2 wamefeli masomo yote waliyofanya katikae ngazi mbalimbali,” álisema.
Katika masomo 34 waliyopimwa watahiniwa, masomo 28 yalifanywa vizuri, masomo 10 yalifanywa kwa wastani na matokeo ya masomo sita yalikuwa mabaya kwa maana ya kuwa chini ya wastani. Aidha watahiniwa watatu wialiibuka Kama watahiniwa bora.