Watakiwa kubuni usalama mifumo ya mitandao

TUME ya Tehama  nchini (ICTC), imesema  ni muhimu  sana vijana  kuwa wataalam pamoja  na  kufanya  bunifu katika maeneo  ya usalama wa mifumo ya mitandao  ili kuwa  na uchumi wa kidigatali wenye kuzalisha  kazi kwao na kufanya Tehama ichangie pato la Taifa.

Mkurugenzi Mkuu wa ICTC, Dk Nkundwe Mwasaga amesema hayo leo  Dar es Salaam wakati akifunga mafunzo  kwa vijana na wanawake wajasiriamali,  kuhusu  namna ya kujilinda pindi wanapokuwa wakifanya mambo mbalimbali ya mtandaoni.

Mafunzo hayo ya siku tatu yaliandaliwa na kuratibiwa na Baraza la Biashara la Afrika Mashariki (EABC) kwa udhamini wa Shirika la Kijerumani la Ushirikiano wa Kimataifa ( GIZ).

Dk Nkundwe amesema kimsingi  mitandao kwa kawaida  inatakiwa iwe na usalama pia kuhakikisha inaaminika kwa mtumiaji wa mwisho, hivyo wajikite kuwa  wabunifu katika eneo hilo, jambo litakalosaidia kukua kwa uchimi wa kidigitali na kusaidia  kuaminika  pia.

“Vijana waoneshe uwezo mkubwa utakaosaidia mifumo kuwa salama, ili watu watakapokuwa wakifanya biashara zao ziweze kuwa salama bila kupoteza vitu vyao na zaidi waweze kuaminika,” amesema Dk Nkundwe.

Amesema mafunzo yaliyotolewa na EABC yanatakiwa kuwa  mengi haswa kwa kuwa  nchi  inajenga uchumi wa kidigitali mkubwa, ambao una nguzo moja ya msingi  inayoelezea mifumo iwe salama na iaminike.

Amesema katika kuhakikisha mifumo inakuwa salama  serikali  imetunga sheria mbalimbali ikiwemo ya  ulinzi wa taarifa binafsi za watu, makosa ya kimtandao ni yapi zote hizo kwa pamoja zikiwa na lengo la kuhakikisha usalama wa mifumo ya kimtandao.

Kwa upande wake Mtendaji  Mkuu wa EABC, John Kalisa amewataka vijana kufanya kazi kwa bidii kuwezesha mifumo ya kimtandao inakuwa salama kwa kuwa ni eneo linaloweza kuwainua kwa kuwapa ajira.

Ametolea mfano nchini Uganda kuwa asilimia 38 ya biashara zilizomo zinaendeshwa na vijana hivyo wajikite kufanya kazi kwa bidii kuwa na kampuni kubwa zinazoweza kutengeneza mifumo ya kutoa ulinzi wa mitandao.

Amesema majukwaa ya mafunzo kama hayo kwa vijana ni eneo linalozalisha ubunifu, wakifanya kazi kwa pamoja kwa ajili ya kukuza uchumi wa kidigitali.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Julia
Julia
1 month ago

I’m making over $7k a month working component time. I saved hearing other people inform me how lots cash they could make online so I decided to look at it. Well, it turned into all proper and has definitely modified my life.
.
.
Detail Here————————————————————–>>>  http://Www.BizWork1.Com

Marry
Marry
1 month ago

Surprising! I’ve been making 100 Dollars an hour since I started freelance on the Internet six months ago. I work long hours a day from home and do the basic work that I get from the business I met online. share this work for you opportunity This is definitely the best job I have ever done………


…Go To This Link…………… > > > > http://Www.Smartcareer1.com

Royal
1 month ago

Google pay 390$ reliably my last paycheck was $55000 working 10 hours out of consistently on the web. My increasingly youthful kinfolk mate has been averaging 20k all through continuous months and he works around 24 hours reliably. I can’t trust how direct it was once I attempted it out. This is my essential concern…:) GOOD LUCK
For more info visit……… http://Www.CareersHome.online  

Karenray
Karenray
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by Karenray
VITA YA MTU NA RWANDA
VITA YA MTU NA RWANDA
1 month ago

Familia ya bwana MAPIGANO/KUTOKUZIKWA YATANGANZA VITA NA NCHI YA RWANDA YA KUBOMOA DARAJA LA MTO KAGERA PALE RUSUMO  KWA KUTUMIA MABOMU YA KUTENGWA KWA MKONO KWA SIKU 5 LENGO NI KUUWA BIASHARA KATI YA TANZANIA NA RWANDA

Capture.JPG
Back to top button
5
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x