Watakiwa kuchangia chakula kwa wanafunzi

KATIKA Kujenga upatikanaji wa elimu bora nchini, jamii imetakiwa kuchangia chakula ili wanafunzi waweze kushiriki vyema katika masomo na kukidhi mahitaji ya elimu nchini.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Meneja miradi wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET,) Martha Makala amesema ni wajibu wa jamii kushiriki katika uboreshaji na upatikanaji wa elimu bora nchini Tanzania.

“Serikali ina nafasi na jamii lazima iangalie namna inavyoweza kuchangia katika kuboresha upatikanaji wa elimu bora nchini ikiwemo kuchangia chakula ili wanafunzi washiriki vyema katika masomo na kuongeza ufaulu…

“Hii pia itasaidia kupunguza vishawishi vinavyosbabisha mimba za utotoni kwa baadhi ya wanafunzi kupokea fedha kwa ajili ya chakula,” amesema.

Pia amesema jamii inatakiwa kushirikiana na serikali za mitaa na asasi za kiraia katika kuhakikisha elimu inakidhi mahitaji ya Taifa kwa kuhakikisha rasilimali zinatumika kwa usahihi.

‘’Mradi huo uliofadhiliwa na Asasi ya Foundation for Civil Society (FCS,) umetekelezwa katika Halmashauri 10 Tanzania Bara uliwalenga wadau katika ngazi ya jamii, halmashauri za wilaya, asasi zinazofanya kazi katika eneo husika, watunga sera na wabunge,”amesema.

Kwa upande wake Mshauri wa Masuala ya Elimu na Maendeleo Japhet Makongo akizungumzia matokeo ya mradi huo taarifa za makadirio ya mapato ya fedha za shule na matumizi zimekuwa hazifahamiki vyema kwa jamii na wazazi.

“Wazazi pia hawana taarifa sahihi na hawashirikishwi katika vipaumbele vya shule ikiwa ni pamoja na mpango na mchakato mzima wa mapato na matumizi pamoja na baadhi vijiji na viongozi wa vijiji kutofuata kalenda ya kuitisha mikutano ya kila mwezi ambapo taarifa kuhusu sekta ya elimu zingewakilishwa,” amesema.

Katika kuhakikisha jamii inakuwa sehemu ya kukuza sekta ya elimu makundi mbalimbali ikiwemo walimu, wazazi na viongozi wa dini wameonesha ushiriki wao katika shughuli za kijamii.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
trackback
1 month ago

[…] mins ago01 mins Home/Jamii/Watakiwa kuchangia chakula kwa wanafunzi Na Brighiter MasakiAugust 2, […]

Darlene Fountain
Darlene Fountain

I make over 13k a month working part-time. I listened to different humans telling me how a good deal of cash they may make online,N255 so I was determined to locate out. Well, it turned into all actual and it absolutely modified my life. Everybody must try this job now by just using this
site….. https://workscoin1.pages.dev/

Last edited 1 month ago by Darlene Fountain
Carol M. Wakefield
Carol M. Wakefield
Reply to  Darlene Fountain
1 month ago

I even have collected $20370 in a period of a month just working part time through apple laptop. 3444 Immediately once I have lost my previous post, I was very upset & thank God I got this easy online job that’s why I was able to have thousands from my home. 2544 Each individual can certainly try this easy offer and may gain more money on-line visiting this
.
.
website___ https://fastinccome.blogspot.com/

AngelaSimmons
AngelaSimmons

Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet… 

Check The Details HERE…..  https://webonline76.blogspot.com/

Last edited 1 month ago by AngelaSimmons
Zambia Revenue Authority
Zambia Revenue Authority
1 month ago

Zambia Revenue Authority

MAPINDUZII.PNG
Back to top button
5
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x