Watu 17 wapoteza maisha ajali ya lori Nigeria

WATU 17 wamekufa na zaidi ya 208 kujeruhiwa baada ya lori lililowabeba kuanguka katika jimbo la Niger nchini Nigeria, kikosi cha usalama barabarani kimeeleza.

Msemaji wa kikosi hicho, Bisi Kazeem amesema ajali hiyo imetokea Jumanne kijiji cha Takalafia eneo la Serikali ya mtaa wa Magama jimboni hapo.

“Waathiriwa waliojeruhiwa wamehamishwa hadi Hospitali Kuu ya Kantagora kwa matibabu ya haraka, waliofariki wapo katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali hiyo hiyo,” Kazeem alisema.

3 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *