Watu 7 wakamatwa wizi miundombinu ya Tanesco Mwanza

KAMANDA wa Jeshi la polisi mkoani Mwanza, Wilbroad Mutafungwa amesema kuwa jeshi lao linawashikilia watu saba kwa kosa la kuiba transfoma na nyaya za umeme mali ya Shirika la Umeme nchini (TANESCO)  wilayani Magu mkoani hapa.

Mutafungwa amesema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake. Amebainisha kuwepo kwa vitendo hivyo vya wizi wa vifaa vya umeme na kuuzwa kwa wauza vyuma chakavu.

Advertisement

Mutafungwa amesema Juni 5, 2023  maeneo ya Sagain wilayani Magu zilipatikana taarifa kuwa wahalifu wameshusha Transforma  na Jeshi la Polisi lilifika kwa wakati na  kumkamata Caroli Clement mwenye  umri wa miaka 26 mkulima na mkazi wa Kisesa.

Kamanda Mutafungwa ameongeza kuwa watuhumiwa wengine waliokamatwa katika msako ni  Daniel Maige ambae ni mkazi wa Igudija K, John Deogratias ambae mkazi wa Nyamhongolo, Baraka Stanley ambae ni mkazi wa  Igoma , Marwa Dismas ambae ni mkazi Kangaye,Wilson Joseph , Ally Tarimo  mkazi wa  kilimahewa.

Mutafungwa ametoa rai kwa wananchi kutoa taarifa pindi wanapoona vitendo vya kihalifu  ili kuweza kutokomeza vitendo hivyo.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *