Watu 700 wafa kwa kipindupindu Zambia

IDADI ya vifo vilivyotokana na mlipuko wa kipindupindu nchini Zambia imeongezeka hadi 700, linasema shirika la matibabu la Médecins Sans Frontières (MSF).

Namba hiyo ni kubwa kuwahi kurekodiwa.

Ilianza katika mji mkuu, Lusaka, mwezi Oktoba na tangu wakati huo imeenea katika majimbo yote ya Zambia na kuwaambukiza watu zaidi ya 19,000.

Advertisement

MSF imesema kipindupindu kinatibika kwa urahisi  kwa kuongezewa maji mwilini  lakini bila uangalizi mzuri mtu anaweza kufa.

“Ugonjwa huu husababishwa na maji machafu, hivyo upatikanaji wa maji safi ya kunywa ni muhimu ili kuuzuia kuenea zaidi”.

Imeeleza taarifa yao