Watu 804 kulipwa Sh bilioni 1.23 kupisha bomba la mafuta

SERIKALI imetumia Sh bilioni 1.23 kwa ajili ya kulipa fidia wananchi 804 waliosaini mikataba ya fidia na kulipwa ili kupisha mradi wa Bomba la Mafuta ghafi wa Afrika Mashariki kwa Mkoa wa Dodoma.
Wananchi hao ni miongoni mwa wananchi 9,813 kutoka mikoa minane inayopitiwa na mradi huo ambapo mpaka Septemba 21, mwaka huu walikuwa wamesaini mikataba ya fidia na kulipwa Sh bilioni 34.89.
Akizungumza jijini Dodoma, Mratibu wa mradi huo kwa upande wa Tanzania kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Asiadi Mrutu alisema waliolipwa ni kati ya wananchi 810 waliopisha mradi huo kwa Mkoa wa Dodoma, hivyo kufanya waliofikiwa na fidia hizo kwa mikoa minane inayopitiwa na mradi huo kufikia asilimia 99.1.
“Katika wananchi waliopisha eneo la mkuza kwa upande wa Dodoma, wananchi 810 wanatakiwa kulipwa fidia na mpaka sasa hivi wananchi 804 wameshasaini mikataba ya fidia na wamelipwa Sh bilioni 1.23,” alisema.
Mikoa inayopitiwa na mradi huo ni Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma, Manyara na Tanga. Alisema pamoja na wananchi hao kulipwa fidia pia wananchi 293 walikubali kujengewa nyumba kulingana na idadi ya nyumba zilizokuwepo kwenye eneo husika wakati wa tathmini na mpaka sasa nyumba 242 zimekamilika kati ya nyumba 339.
Alisema pia TPDC kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wameweka alama za mipaka kwenye eneo la mkuza lenye kilometa 612.33 kati ya kilometa 1,147 sawa na asilimia 53.39.
Akizungumzia fursa za ajira wakati wa utekelezaji wa mradi huo, Mrutu alisema mpaka Juni 30, mwaka huu Watanzania 3,619 wameajiriwa sawa na asilimia 91 ya wafanyakazi wote.
Mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga, Tanzania lina urefu wa kilometa 1,443 na unatarajia kugharimu Dola za Marekani bilioni 5.088 na litakuwa na uwezo wa kupitisha mapipa 216,000 kwa siku utakapoanza kazi.
Muda wa ujenzi wa mradi huo ni miezi 24 na unatarajia kuanza kutekelezwa Januari mwakani. Kuhusu kazi za awali zinazoendelea, Mrutu alisema kwa sasa kwa upande wa Tanzania ni ujenzi wa makambi ya ujenzi ambapo makambi manne kati ya 12 yamekamilika kwa asilimia 100.
Pia ujenzi wa karakana ya kuandaa mabomba eneo la Sojo mkoani Tabora umefikia asilimia 40 na umetoa ajira kwa Watanzania 426 sawa na asilimia 95 na kampuni 20 za Kitanzania zimetoa huduma zenye thamani ya Sh bilioni 50.
WIZARA YA NDOTO
HOTUBA YA WIZARA YA NDOTO
ULIMWENGU WA NDOTO
One. DEREVA BODABODA ANA NDOTO YA KUMILIKI KAMPUNI YA NDEGE
Two. MUUZA MBOGAMBOGA ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA MBOGA MBOGA
Three. MUUZA VITUNGUU SUMU ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA VITUNGUU SUMU
Four. MUUZA NYANYA ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA NYANYA
Five. MUUZA MAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA NDEGE
Six. MUUZA BAR ANA NDOTO YA KUMILIKI KUJENGA BAR
Seven. MUUZA FREMU ANA NDOTO YA KUMILIKI SHOPPING MALLS
Eight. MGANGA WA KIENYEJI ANA NDOTO YA KUMILIKI HOSPITALI
Nine. MPIGA DEBE ANA NDOTO ZA KUMILIKI KAMPUNI YA MABASI
Ten. MAMA NTILIE ANA NDOTO YA KUMILIKI HOTELS
Eleven. MCHEKESHAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KITUO CHA TELEVISION
Twelve. MTANGAZAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KITUO CHA TELEVISION
Upo sahihi “tukasomeeeeeee tueleweeeeeee Saaaana
Fursa BABA YETU ULIE MBINGUNI NA BWANA YESU ASIFIWE – IMPORT WATU FROM US TO TZ……..
UKIKUTANA NA MZUNGU AKUPE BRIEFCASE YA HELA UTEKELEZE VYOTE MWENYEWE
WIZARA YA NDOTO
HOTUBA YA WIZARA YA NDOTO
ULIMWENGU WA NDOTO
One. DEREVA BODABODA ANA NDOTO YA KUMILIKI KAMPUNI YA NDEGE
Two. MUUZA MBOGAMBOGA ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA MBOGA MBOGA
Three. MUUZA VITUNGUU SUMU ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA VITUNGUU SUMU
Four. MUUZA NYANYA ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA NYANYA
Five. MUUZA MAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KIWANDA CHA NDEGE
Six. MUUZA BAR ANA NDOTO YA KUMILIKI KUJENGA BAR
Seven. MUUZA FREMU ANA NDOTO YA KUMILIKI SHOPPING MALLS
Eight. MGANGA WA KIENYEJI ANA NDOTO YA KUMILIKI HOSPITALI
Nine. MPIGA DEBE ANA NDOTO ZA KUMILIKI KAMPUNI YA MABASI
Ten. MAMA NTILIE ANA NDOTO YA KUMILIKI HOTELS
Eleven. MCHEKESHAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KITUO CHA TELEVISION
Twelve. MTANGAZAJI ANA NDOTO YA KUMILIKI KITUO CHA TELEVISION
Upo sahihi “tukasomeeeeeee tueleweeeeeee Saaaana
Fursa BABA YETU ULIE MBINGUNI NA BWANA YESU ASIFIWE – IMPORT WATU FROM US TO TZ……..
UKIKUTANA NA MZUNGU AKUPE BRIEFCASE YA HELA UTEKELEZE VYOTE MWENYEWE..
KWELI WEWE JAMAA KWAKO HAKUNA BAG
TUNZA MAZINGIRA YAKUTUZE… UTAKACHOONDOA NDIO KAZI..
100% KIWEKWACHO HUMO HUTENGENEZWA NA WANAWAKE
file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg
file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image004.jpg