Watuhumiwa wanne wa ujambazi wadakwa Dar

JESHI  la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limewakamata majambazi sugu wanne maeneo ya Mabibo External  na kwa sasa watuhumiwa hao wamelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Akizungumza leo Januari 9,2023, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, ACP Jumanne Muliro amesema watuhumiwa hao hali zao ni mbaya baada ya kujeruhiwa kwa risasi wakati wakishambuliana na Polisi .

“Majambazi hao wamekamatwa Januari 8 mwaka huu wamekiwa wakituhumiwa kujihusisha  na vitendo vya kihalifu vya unyang’anyi wa kutumia silaha na kupora fedha  katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaamna na mikoa ya jirani.” Amesema Muliro

Muliro amewataja viongozi wa  watuhumiwa hao wa  ujambazi sugu ni Athuman Mbalilo maarufu kwa jina Soti(50)Mkazi wa Kimara Temboni na Mpoki Raphael kwa jina lingine Mwangwisya(41) mkazi wa Mbezi Luis.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments
Back to top button
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x