Waviu Kibaha kufunga ndoa 2024

WENZA, Vaileth Kawovela na Evodius na Gozbelt wakazi wa Kibaha, mkoani Pwani wanaoishi na Virusi vya Ukimwi  wanaonufaika na huduma za matunzo kupitia Taasisi  Tanzania Health  Promotion Support (THPS) wanatarajia kufunga ndoa mwaka 2024.

Wamesema hayo walipozungumza na gazeti hili kwenye maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani Disemba mosi mwaka huu ambapo kitaifa yalifanyika mkoani Morogoro.

Wenza watarajiwa hao waliishukuru Taasisi  THPS  inayosimamia mradi wa  Kituo cha Kimarekani cha Kudhibiti Magonjwa ( CDC) chini ya Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na UKIMWI, (PEPFAR) na Afya hatua kwa kuweza kuwafikisha hapo walipofikia.

Advertisement

Kawovela ambaye ni mama mtarajiwa alisema , THPS imeweza kumlea yeye kuanzia akiwa mtoto hadi sasa akwia amefikisha umri wa miaka 24  baada ya kuzaliwa na maambukizi hayo , na kupatiwa huduma rafiki  tangi  akiwa mtoto .

‘ Hatua hii iliendelea kunipa  furaha na kufarijika kwani Taasisi hii  imeweza kunileta  tangu nikiwa  na umri  mdogo  hadi sasa nimefikisha umri wa miaka 24 “ alissema Kawovela .

Kawovela alisema  THPS ilikuwa inatoa huduma rafiki kuanzia alipokuwa na umri ndogo alipokuwa akifikishwa  kwenye kituo cha  Afya kwa ajili ya kliniki ya kupata dawa huku akichanganywa kucheza na watoto wengine.

“ Tulikuwa tunacheza na watoto wenzetu na wao walikuwa wanatusukuma kwenye bembea  na wanatugawia  pipi  na maziwa”, ilinipa   furaha kwa vile tunakutana na watoto wengine huku wao wakituhumiza  sisi ( watoto)  tusiachekunywa dawa ili tuwe na afya nzuri “ alisisitiza  Kawovela.

Kawovela alisema,  wakati mwingine watumishi hao walitumia mbinu za  kuchukua mfano wa dawa sijui ni za kutuliza maumivu  na kuzimeza  mbele ya watoto na  kitendo hicho kilikuwa kuonesha  hakuna madhara yoyote.

Alisema  kitendo hicho kiliwahamasisha wao ( watoto)  kujenga shauku  ya kupenda kwenda  Kituo cha Afya  kila mwisho wa mwezi kukutana  na watoto wenzao  ili wapatiwe  maziwa na pipi.

Alisema ,tangu kipindi hicho ameendelea  kunufaika na huduma rafiki kwa vijana ambazo zimeendelea kumsaidia  kukua kiakili , kujitambua na kuchangamana na vijana vituo vingine na  kuona ya kwamba hayupo pekee yake.

Kawovela alisema  ,kupitia mradi huo ulianzisha  klabu zao  na   pia kupitia klabu za vijana chini ya mradi huo zimemwezesha  kukutana na mwenza wake  , kuendelea kutambuana zaidi  na hatimaye  kuwa na mahusiano ( mapenzi) .

“ Mpaka sasa hivi tunatarajia kufunga ndoa mwakani Mungu akipenda na pia tunatarajia kupata mtoto siku za karibuni “ alisema  Kawovela .

Alisema  anamshukuru Mungu kwa sasa yenye ni mama mtarajiwa ambapo  anaendelea  kupata mafundisho  na elimu  ili niweza kumzaa mtoto wangu akiwa salama.

“… japo kuwa hata sasa yapo maelekezo ambayo ninapewa ili niweze kuzaa mtoto salama  ambaye  hatakuwa na  maambukizi” alisema Kawovela

Anasema mafundisho na elimu anayopewa ni kwa ajili ya kupewa tahadhari kuhusu mkumkinga  mtoto na maambukizi wakati wa ujauzito , kuzaliwa na wakati wa kunyoyesha .

“ Wakati wa ujauzito ukipata haya mafunzo ndipo tunazungumzia mtoto amezaliwa …jambo kubwa unapewa tahadhari dawa za kinga ambazo anapewa mtoto asije akapata maambukizi wakati wa kumyonyesha “ alisema  Kawovela .

“…anazitumia hizo dawa na baada ya miezi kadhaa anapimwa afya yake , mara ya kwanza , ya pili nay a tatu na kuthibitishwa kama hanaa maambukizi  basi anaendelea na maisha yake “ alisema  Kawovela .

Kwa upande mume mtarajiwa wa Kawovela, Evodius   Gozbelt,  ambaye ni mkazi wa mkoa wa Pwani , anashukuru ufadhili uliotolewa na kuendelea , umewatoa sehemu moja na kuwafikisha sehemu salama.

Alisema kwake kutokana misaada hiyo na klabu zinazosimamiwa na Taasisi hiyo imemwezesha kupata mchumba ambaye anatarajia kufunga naye ndoa mapema mwakani (2024) ingawa kwa sasa ni wakati wowote anatarajia kujifungua mtoto.