Wazee CCM Iringa wazungumzia bandari

WAZEE wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa wametangaza kuishiwa na uvumilivu na kuamua kulaani vikali mwenendo wenye viashiria vya kisiasa unaotishia kuigawa nchi kupitia matamko na maoni mbalimbali yanayotolewa kuhusu suala la uwekezaji wa bandari.

Pamoja na bandari, wazee hao wamesema wao pia ni sehemu ya Watanzania wanaounga mkono maridhiano ya vyama vya siasa yaliyoanzishwa na Rais Samia Suluhu Hassan lakini yatawafanya wasikae kimya na hata kutoa ushauri mgumu pale watakaposikia baadhi ya wanasiasa wakiyatumia kumdhihaki na kumkashfu Rais.

Kupitia tamko lao lililotolewa mjini Iringa leo na Mwenyekiti wa Wazee wa CCM Mkoa wa Iringa, Aman Mwamwindi mbele ya wawakilishi wa wazee wa kata zote 18 za mjini Iringa, wazee hao wamesema kwa nia njema Rais alitoa fursa kwa wananchi wake kutoa maoni kuhusiana na uwekezaji huo wa bandari.

“Inasikitisha kuona baadhi ya watu wamechukulia mjadala huu kwa dhamira za kuigawa nchi kikanda na kidini. Wazee tunakemea kwa nguvu zote tabia hii inayoweza kusababisha kuvunjika kwa Amani, utulivu, umoja na mshikamano wa nchi tuliorithi kutoka kwa waasisi wetu Mwalimu Julius Nyerere na Sheik Abeid Amani Karume,” amesema.

Mwamwindi amesema wazee wa mkoa wa Iringa wanawashauri watoa maoni watumie lugha ya staha huku wakijali uzalendo na sio maslai binafsi.

“Sisi wazee wa mkoa wa Iringa tupo pamoja na Rais Samia Suluhu Hassan na serikali yake na tunaunga na tutaunga mkono uwekezaji wowote ule ili mradi ufanyike kwa maslai ya Taifa letu,” amesema.

Kuhusu maridhiano ya kisiasa, wazee hao wamevitaka vyama vya siasa kupitia kauli mbalimbali zinazotolewa na viongozi au wanachama wao kuheshimu mamlaka ya Rais na kutumia lugha zinazoendana na hadhi hiyo ili kulinda, kuheshimu na kuiendeleza dhamira njema inayokusudiwa katika maridhiano hayo.

 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Daudi Yasin aliyehudhuria shughuli hiyo kama mwalikwa amesema wanachama na wapenzi wa CCM wa Mkoa huo wanaimba wimbo mmoja katika uwekezaji wa bandari wakiamini jambo hilo lina nia njema na litakuwa na manufaa makubwa kwa maendeleo ya Taifa.

“Serikali imeamua kuwekeza katika jambo hili, kwa ufafanuzi na elimu inayoendelea kutolewa kuhusu uwekezaji huu hatuna mashaka kwamba jambo hili lina nia njema. Tusiwasikilize watu wanaopotosha,” amesema.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
julizaah
julizaah
1 month ago

I made over $700 per day using my mobile in part time. I recently got my 5th paycheck of $19632 and all i was doing is to copy and paste work online. this home work makes me able to generate more cash daily easily simple to do work and regular income from this are just superb. Here what i am doing.

.

.

.

Check info here——————>>> http://www.join.salary49.com

Last edited 1 month ago by julizaah
Darlene Fountain
Darlene Fountain
1 month ago

I make over 13k a month working part-time. I listened to different humans telling me how a good deal of cash they may make online,N255 so I was determined to locate out. Well, it turned into all actual and it absolutely modified my life. Everybody must try this job now by just using this
site….. https://workscoin1.pages.dev/

Last edited 1 month ago by Darlene Fountain
AngelaSimmons
AngelaSimmons
1 month ago

Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet… 

Check The Details HERE…..  https://webonline76.blogspot.com/

Last edited 1 month ago by AngelaSimmons
Zambia Revenue Authority
Zambia Revenue Authority
1 month ago

Zambia Revenue Authority

MAPINDUZII.PNG
Back to top button
4
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x