Wenger awasili Tanzania kuishuhudia Simba SC

MKUU wa maendeleo ya soka kutoka Shirikisho la Soka Ulimwenguni (FIFA) Arsene Wenger amewasili Tanzania kushuhudia mchezo wa AFL kati ya Simba SC dhidi ya Al-Ahly uwanja wa Mkapa Dar es Salaam.

Wenger ambaye aliwahi kuifundisha klabu ya Arsenal ya England kwa mafanikio makubwa amewasili muda huu akiwa na baadhi ya watu wake wa karibu.

Mwamuzi mstaafu wa FIFA Pierluigi Collina ni miongoni mwa waliowasili pia

Advertisement

Viongozi ambao mpaka sasa wameshawasili ni Rais wa Fifa, Gianni Infantino na wengine ambao wote wataelekea uwanja wa Mkapa kwa mchezo huo.

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *