‘Wenye mapenzi na uandishi wakasome’

‘Wenye mapenzi na uandishi wakasome’

MSEMAJI Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa  amesema kazi ya uandishi wa habari hapa nchini inasimamiwa na sheria ya huduma za vyombo vya habari sura namba 229,na kwamba hakuna mtu anayeruhusiwa kutumia vyombo vya habari kwa maslahi yake binafsi

Akizungumza katika kongamano la maadhimisho ya miaka 30 ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani mjini  Unguja, Msigwa  amesema kuna baadhi ya watu wamekuwa  wakifanya mzaha na tasnia ya habari, jambo ambalo halitavumiliwa.

“ Tasnia ya uandishi wa habari haifungi milango  kwamba mtu  mwingine haruhusiwi  kwenda,  muhimu ni kuzingatia maadili ya uandishi, miiko ya uandishi wa habari misingi ya uandishi wa habari, tunachotoa wito kwao waende kwenye vyuo vipo watasoma watapandikizwa taaluma,” alisema Msigwa.

Advertisement

Kuhusu ulinzi wa waandishi wa habar, Msigwa  amesema serikali haijawahi kufumbia macho ulinzi wa vyombo vya habari nchini.

Hatahivyo amewaon ya wamiliki wa vyombo  ambao wanakataa  kuwaajiri waandishi wa habari wanawake  na kusema ni kosa la kisheria.

“ Ni vizuri waandishi wa habari wanawake wakatambua kwamba wanapofanya kazi hii si suala la  kazi yake la ajira yake tu,  lakini ajue kwamba amebeba majukumu  zaidi ya kusimamia mambo mengi ya wanawake ambao sio waandishi wa habari,  kwa hiyo ni kazi ambayo mimi nasema ni wito na waandishi wa habari wanawake naona  agenda za wanawake  zina watu wa kuzisukuma,” alifafanua Msigwa.

Kongamano hilo linataraji kufikia  kielle chake hii leo Mei 3, 2022, ambapo  Tanzania inaungana na nchi nyingine duniani kuadhimisha  siku ya  uhuru wa vyombo vya habari duniani.