Wiki moja yaokoa maisha watoto 427 JKCI

WATOTOT 427 wenye matatizo ya matundu kwenye moyo, matatizo ya mishipa ya damu na Valve za moyo wamefanyiwa uchunguzi katika kambi ya matibabu ya wiki moja Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es Salaam.

Kati ya watoto hao 41 walifanyiwa upasuaji kwa njia ya tundu dogo ambao umefanyika kupitia mtambo wa Cathlab na watoto 18 wamefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo wa kufungua kifua.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa kambi hiyo, Mkurugenzi wa Upasuaji wa JKCI,  Dk Angela Muhozya, alisema kambi hiyo ilianza Mei 12 hadi 19,  ambapo JKCI kwa kushirikiana na madaktari kutoka Mradi wa Little Heart wa Shirika la Muntada Aid kutoka London,Uingereza.

“Hawa ni madaktari ambao wamekuwa wakija katika Taasisi ya moyo kwa miaka saba mpaka sasa na wanakuja kwa ajili ya matibabu ya magonjwa ya moyo kwa watoto na kwa kawaida wakija huwa tunafanya uchunguzi kwa watoto wengi na wengine wanapitiwa huduma za upasuaji,” amesema.

Amesema  watoto 18 waliofanyiwa upasuaji wengine wameshatoka chumba cha uangalizi maalum, ambapo wamebakiwa  watoto watatu.

“Tunawashukuru sana wenzetu kwa kuendelea kufanya kazi na JKCI kwanza wanatujengea uwezo kila mwaka tunaenda hatua mbele na pia wanatuletea vifaa katika kila walichotuelekeza wakirudi tumepiga hatua zaidi,”amesema.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
neknoyirze
neknoyirze
4 months ago

Online, Google paid $45 per hour. Nine months have passed since my close relative last had a job, but in the previous month she earned $10500 by working 8 hours a day from home. Now is the time for everyone to try this job by using this website…

Click the link—↠  http://www.join.hiring9.com

Last edited 4 months ago by neknoyirze
Back to top button
1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x