Wizara ya Elimu, TET, GMOE, GERIS kuimarisha Tehama

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WyEST) kupitia Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na Ofisi ya Elimu ya Gwangju Metropolitan (GMOE) kupitia Global Education and Research Information Service (GERIS) zimesaini hati ya makubalino ya miaka minne katika mradi wa kuimarisha matumizi ya TEHAMA nchini.

Hati hizo zimesaini leo Novemba 7, 2023 jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji.

Akizungumza Mkurugenzi Mtendaji wa TET, Dk Anneth Komba amesema makubaliano matatu yaliyofikiwa ni ofisi ya Elimu ya Gwangju itaipatia Taasisi ya Elimu kila mwaka kompyuta na vifaa vingine vya TEHAMA na TET itawajibika kulipia gharama za kuvikomboa vifaa hivyo bandarini pamoja na na gharama ya kuvisafirisha katika shule husika.

Pia, Gwangju itaandaa na kuwaalika kuhudhuria mafunzo nchini Korea wataaluma, walimu na watumishi wengine wa umma kutoka wizara ya Elimu juu ya matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji pamoja na mambo mengine ya Kielimu. Mafunzo haya yatafadhiliwa na Ofisi ya Elimu ya Gwangju ikiwemo tiketi ya kwenda na kurudi nchini Korea, chakula na malazi nchini Korea.

“Ofisi ya Elimu ya Gwangju itatoa wataalamu kuja Tanzania kutoa mafunzo na itabeba gharama zote za mafunzo hayo ikiwemo gharama za safari ya kuja na kurudi na malazi,”amesema.

Naye, Kamishna wa elimu wa Gwangju, Lee Wang Do akizungumza amesema Tanzania ina fursa na rasilimali nyingi ikiwemo Mlima Kilimanjaro na mbuga za Wanyama kama Ngorongoro, Serengeti na nyingine, ametembelea shule ya Tegeta A na kwamba mazingira waliyoyakuta ni kama shule za Korea Kusini miaka 50 iliyopita.

“Korea pia zilikuwa hivi hivi lakini ukiwa na nia na hari, mkawa na ndoto za kufikia malengo basi mtafanikiwa, hata Korea iliwahi kusaidiwa na nchi zilizoendelea, lakini wananchi tuliamua kufanya kazi kwa bidii ndio Korea mnayoiona leo, naamini kama Tanzania inataka kupiga hatua basi mkichukua Korea kama mfano ‘role model’ katika TEHAMA tutashukuru sana.”Amesema.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
JenniferTate
JenniferTate
24 days ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 24 days ago by JenniferTate
Julia
Julia
24 days ago

I’ve got my first check for a total of 13k dollars. I am so energized, this is whenever I first really acquired something. I will work much harder now and I can hardly hang tight for the following week installment.
.
.
Detail Here——————————————————–>>>  http://Www.BizWork1.Com

Angila
Angila
24 days ago

I have just received my 3rd paycheck which said that $16285 that i have made just in one month by working online over my laptop. This job is amazing and its regular earnings are much better than my regular office job. Join this job now and start making money online easily by
.
.
.
.
Just Use This Link……..> > > http://Www.Smartcareer1.com

babofe8659
23 days ago

JOIN US I’m making a good salary from home 16580-47065/ Doller week , which is amazing under a year ago I was jobless in a horrible economy. I thank God every day I was blessed with these instructions and now it’s my duty to pay it forward and share it with Everyone,
Here is I started.…………> http://profitguru7.com

Back to top button
4
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x