Zimamoto waonya wanaotoa taarifa za uwongo

Jeshi la Zimamoto na uokoaji  mkoani Arusha limewaonya wananchi wanaotoa taarifa za uongo kwa jeshi hilo, likisema linahitaji ushirikiano kutoka kwa wananchi, lli liweze kutimiza malengo yake

Limesema pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa na jeshi hilo mkoani Arusha kwa kutoa elimu kwa wananchi, bado kuna changamoto kubwa ya watu wasiokuwa na nia njema wanapiga simu na kutoa taarifa za uongo  ofisi za jeshi hilo za majanga

Akizungumza na HabariLEO, Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Arusha, Osward Mwanjejele amesema kwamba taariza za uongo wanazozipokea kutoka kwa watu mbalimbali  jijini Arusha zinazilifedhehesha jesho hilo

Advertisement

“Kwa kweli taarifa za majanga kutoka kwa watu wasiowaaminifu, zinatufedhehesha sana maana tunatumia rasilimali zetu na nguvu nyingi  kwenda kwenye tukio. Unapofika kwenye tukio hukuti chochote,”  amesema

Amesema katika kipindi cha miezi ya karibuni jeshi hilo lilipokea simu 8 kutoka kwa watu mbalimbali wakilifahamisha jeshi hilo kuwa kuna matukio ya majanga.

“Watu watupe ushirikiano, wasipambane na matukio na watoe taarifa za kweli,” alisema

Amesema kwamba  karibu mwaka mzima jeshi hilo limekuwa likitoa elimu kwa umma kuhusu masuala yanayohusu majanga ya moto na uokoaji katika Mkoa wa Arusha.

“Tumekuwa tukitumia vyombo vya habari hasa magazeti, redio na televisheni katika kutoa elimu kwa umma. Pia tunatumia na majukwaa mbalimbali kama vikao vya madiwani, kwenye maonesho na pia wakati mwingine huwa tunaalikwa kwenye mikutano ya serikali za mitaa,” amesema.

Pia ametoa ushauri kwa wananchi  kuchukua tahadhari mapema na kuepukana na matumizi holela ya mitungi ya gesi  nyumbani, pia katika uchimbaji wa visima ambavyo wakati wa mvua vinajaa maji na kusababisha   vifo.

5 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *