Wakazi wa kijiji cha Shilela wanufaika na mradi mpya wa maji

SHINYANGA: WANANCHI 1,250 wa kijiji cha Shilela Halmashauri ya Msalala Wilayani Kahama mkoani Shinyanga wameanza kunufaika kwa mradi wa maji safi uliotumia zaidi ya Sh milioni 91.7. mpaka kukamilika kwake.
Meneja wa Wakala wa Majisafi na Mazingira Vijijini (Ruwasa) Wilaya ya Kahama, Mhandisi Magili Maduhu amesema hayo leo wakati akitoa taarifa mbele ya kiongozi wa mbio za mwrnge wa Uhuru kitaifa Wazo Mwang’onda.
Mhandisi Maduhu amesema chanzo cha upatikanaji wake ni kisima kirefu chenye urefu wa mita 71.2 na uwezo wa ujazo wa lita 1400. ikiwemo ujenzi wa mnara wa kioski cha kuchotea maji na kusimika simtanki lita 1000.

Mwang’onda amesema mradi huo wa maji wananchi wanatakiwa wautunze ili uendelee kuwanufaisha kwani serikali imetumia fedha nyingi kutaka wananchi wapate maji safi na salama.



