ABC yaiduwaza Savio kikapu Dar

DAR ES SALAAM; ABC imepata ushindi wa pointi 68-65 dhidi ya Savio katika mchezo wa Ligi ya Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam uliochezwa jana usiku Uwanja wa Don Bosco, Upanga.
–
Mchezo huo ulikuwa wa ushindani mkubwa, huku timu hizo zikibadilishana uongozi katika robo mbalimbali kabla ya ABC kupata pointi muhimu katika robo ya mwisho na kuondoka na ushindi.
–
Savio ilianza vizuri kwa kuongoza robo ya kwanza kwa pointi 20-15, lakini ABC ikapunguza pengo katika robo ya pili na kufikia mapumziko ikiwa nyuma kwa pointi moja tu, 31-32.
–
Robo ya tatu iliendelea kuwa ya kusisimua, ABC ikigeuza matokeo na kuingia robo ya mwisho ikiwa mbele kwa pointi 48-47.
–
Katika robo ya nne, ABC ilidhibiti mchezo na kufikisha pointi 68, huku Savio ikimaliza ikiwa na pointi 65.
Katika mchezo mwingine, Twalipo Queens iliibuka na ushindi wa pointi 47-31 dhidi ya Mgulani Queens.



