TISEZA, TLS–AYL kuboresha huduma za kisheria wawekezaji

DAR ES SALAAM; Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) imesaini makubaliano ya ushirikiano wa miaka mitatu na Chama cha Mawakili Vijana ndani ya Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS–AYL), yatakayolenga kuimarisha huduma za kisheria kwa wawekezaji, kuwajengea uwezo mawakili vijana na kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini.

Makubaliano hayo yanatarajiwa kuwawezesha mawakili vijana kushiriki kikamilifu katika utoaji wa huduma za kisheria zinazohusiana na uwekezaji, huku yakifungua fursa zaidi za ushiriki wao katika shughuli za maendeleo ya uchumi na uwekezaji.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya utiaji saini wa makubaliano hayo jijini Dar es Salaam Julai 29, Mkurugenzi Mtendaji wa TISEZA, Gilead Teri, amesema ushirikiano huo utaunganisha nguvu za taasisi hizo katika kuwajengea uwezo mawakili vijana kupitia mafunzo ya sheria za uwekezaji, ujasiriamali na mbinu za kisasa za utoaji wa huduma za kisheria kwa wawekezaji.

 

Amesema kupitia ushirikiano huo, mawakili vijana pia watashiriki katika maboresho ya sera, sheria na mifumo inayosimamia uwekezaji nchini, hatua ambayo itasaidia kuongeza ufanisi wa huduma kwa wawekezaji na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha kuvutia uwekezaji wa ndani na nje ya nchi.

Teri amesema lengo la makubaliano hayo ni kuhakikisha mawakili vijana wa Kitanzania hawabaki kuwa waandishi wa mikataba pekee, bali wanajengewa uwezo wa kuwa wataalamu wa sheria za uwekezaji watakaoweza kutoa ushauri wa kitaalamu kwa wawekezaji na kuchangia mageuzi ya uchumi wa taifa.

Aidha, amesema ushirikiano huo utapanua fursa za ajira na maendeleo ya kitaaluma kwa mawakili vijana, sambamba na kupunguza gharama za huduma za kisheria kwa wawekezaji kupitia upatikanaji wa wataalamu wengi wenye ujuzi katika masuala ya uwekezaji.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Umoja wa Mawakili Vijana ndani ya Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS–AYL), Wakili Emmanuel Ukashu, amesema wamechagua kushirikiana na TISEZA kwa kutambua kuwa uwekezaji ni miongoni mwa nguzo muhimu za maendeleo ya uchumi wa Tanzania.

Amesema makubaliano hayo ya miaka mitatu yatawapa mawakili vijana fursa ya kupata mafunzo ya kina kuhusu sheria za uwekezaji, kuongeza uwezo wao wa kitaaluma na kushiriki moja kwa moja katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.

Ukashu ameongeza kuwa ushirikiano huo utaimarisha uhusiano kati ya sekta ya sheria na sekta ya uwekezaji, hatua itakayochangia kujenga mazingira yenye uwazi, uhakika wa kisheria na ushindani, ambayo ni muhimu katika kuvutia wawekezaji na kuchochea ukuaji endelevu wa uchumi wa Tanzania.

Habari Zifananazo

16 Comments

  1. Woah! I’m really enjoying the template/theme of this site.
    It’s simple, yet effective. A lot of times it’s difficult to get
    that “perfect balance” between superb usability and appearance.
    I must say you have done a very good job with this. Also, the blog loads extremely fast
    for me on Safari. Excellent Blog!

  2. ข้อมูลชุดนี้ อ่านแล้วเข้าใจง่าย ครับ
    ผม ได้อ่านบทความที่เกี่ยวข้องกับ หัวข้อที่คล้ายกัน
    ที่คุณสามารถดูได้ที่ betflixclub
    น่าจะถูกใจใครหลายคน
    มีการยกตัวอย่างที่เข้าใจง่าย
    ขอบคุณที่แชร์ ข้อมูลที่มีประโยชน์ นี้
    และหวังว่าจะมีข้อมูลใหม่ๆ มาแบ่งปันอีก

  3. Woah! I’m really loving the template/theme of this blog.
    It’s simple, yet effective. A lot of times it’s hard to get that “perfect balance” between user
    friendliness and visual appeal. I must say you’ve done a amazing job with
    this. Also, the blog loads very fast for me on Safari.
    Outstanding Blog!

  4. Usually I don’t learn article on blogs, however I wish to say that this write-up very compelled me to try and do it!
    Your writing style has been amazed me. Thanks, quite great post.

  5. Do you have a spam issue on this website; I also am a blogger, and I was wanting to know your situation; we have created some nice procedures and we
    are looking to swap methods with other folks, please shoot me an email
    if interested.

  6. I love your blog.. very nice colors & theme. Did you make this website yourself or did you hire someone to do it for
    you? Plz respond as I’m looking to create my own blog and would like to find out where u got this from.
    thank you

  7. Wow, wonderful weblog layout! How long have you ever been running a blog for?
    you make running a blog look easy. The full look of your web site is excellent, as neatly as
    the content!

  8. This partnership between TISEZA and legal institutions to train young lawyers in investment law, entrepreneurship, and modern legal services is a strategic investment in Tanzania’s economic development. For law firms, legal training institutions, and business development organizations that want to present training materials, program guides, or professional resources with clarity, a reliable acrylic display stand supplier can help ensure your physical materials reflect the same level of professionalism and commitment to capacity building.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button