Vijana wasisitize kwa na maono ya maisha

SHINYANGA: VIJANA wametakiwa kuwa na maono ya maisha na kutumia mitandao ya kijamii kutafuta fursa za maendeleo badala ya kutumia muda mwingi kuangalia machapisho na kutuma ujumbe usio na staha.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Frank Nkinda, wakati akifungua Jukwaa la Vijana la Halmashauri ya Msalala lililowakutanisha zaidi ya vijana 250.

Nkinda amesema kila kijana anapaswa kuwa na maono yake binafsi na kuyafanyia kazi ili kufikia malengo, akisisitiza kuwa simu za mkononi na mitandao ya kijamii zinaweza kuwa nyenzo muhimu za kupata fursa za kielimu na kiuchumi.

“Unaamini kijana mwenzangu, Tanzania ya kesho ni mimi na wewe. Hivyo tuilinde kwa amani na upendo na tutumie vizuri simu zetu za mkononi kupata fursa za kimaendeleo,” amesema Nkinda.

Amesema Serikali inataka kuona vijana wakiwa na maono yanayojenga, akitoa mfano kwa wanafunzi kuzingatia masomo yao na kuweka malengo ya taaluma wanazotaka kufikia, ikiwamo udaktari, uongozi na sekta mbalimbali za uchumi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala, Rose Manumba, amesema jukwaa hilo ni fursa kwa vijana kukutana, kubadilishana mawazo na kujenga uzalendo kwa kuwa kila mmoja ana nafasi katika ujenzi wa taifa.

Naye Ofisa Vijana kutoka Halmashauri ya Bariadi na mwezeshaji wa jukwaa hilo, Godwin Misana, amesema uadilifu ni msingi muhimu kwa kijana anayelenga kufanikiwa.

Amesema kijana anaweza kuwa na uwezo mkubwa wa kitaaluma au kufanya vizuri kazini, lakini bila uadilifu anaweza kupoteza fursa, hivyo amewataka vijana kutanguliza uzalendo, uadilifu na uwajibikaji katika maisha yao.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button