Wakazi wa kijiji cha Shilela wanufaika na mradi mpya wa maji

SHINYANGA: WANANCHI 1,250 wa kijiji cha Shilela Halmashauri ya Msalala Wilayani Kahama mkoani Shinyanga wameanza kunufaika kwa mradi wa maji safi uliotumia zaidi ya Sh milioni 91.7. mpaka kukamilika kwake.

Meneja wa Wakala wa Majisafi na Mazingira Vijijini (Ruwasa) Wilaya ya Kahama, Mhandisi Magili Maduhu amesema hayo leo wakati akitoa taarifa mbele ya kiongozi wa mbio za mwrnge wa Uhuru kitaifa Wazo Mwang’onda.

Mhandisi Maduhu amesema chanzo cha upatikanaji wake ni kisima kirefu chenye urefu wa mita 71.2 na uwezo wa ujazo wa lita 1400. ikiwemo ujenzi wa mnara wa kioski cha kuchotea maji na kusimika simtanki lita 1000.

Mwang’onda amesema mradi huo wa maji wananchi wanatakiwa wautunze ili uendelee kuwanufaisha kwani serikali imetumia fedha nyingi kutaka wananchi wapate maji safi na salama.

Habari Zifananazo

One Comment

  1. Cash earning job to earns more than $700 per day. getting paid weekly more than $3500 or more simply doing easy work online. no special skills required for this job and regular earning from this are just awesome. all you need is 2 hrs a day for this job and earning are awesome. every person can get this by follow details here…

    THIS→→→→ http://Www.Payathome1.com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button