TBS yapongezwa udhibiti usalama, ubora wa bidhaa

DODOMA; Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda,Biashara,Kilimo na Mifugo imeipongeza TBS kwa kutekeleza majukumu yake ya udhibiti ubora kwa ufanisi.

Pongezi hizo zimetolewa na  Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Deogratias Mwanyika wakati wa kikao cha Kamati cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu,katika, ofisi za Bunge jijini Dodoma mapema  leo.

Mwanyika amesema juhudi zinazofanywa na TBS kuhakikisha usalama na ubora wa bidhaa zinazotumiwa na Watanzania zinaonekana  na kutoa rai kwa TBS kuendelea kutoa elimu na kuongeza jitihada sambambana na kuwa na programu maalumu za kushughulikia bidhaa zinazoingizwa nchini kwa njia zisizo rasmi.

Kwa upande wake Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, ameishukuru kamati hiyo na kuahidi kufanyia kazi maelekezo na ushauri uliotolewa na kamati,  ili kuendelea kurahisisha utendaji kazi wa TBS.

Amesema lengo la wizara kupitia TBS ni kuhakikisha kunakuwa na bidhaa zenye ubora na usalama katika soko zinazozalishwa  ndani na zinazotoka nje ya nchi.

 

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button