Kocha wa viwango kuja Tanzania kuinua waogeleaji

DAR ES SALAAM: Mkurugenzi wa Monti International School, Fatma Fernandez, amesema shule hiyo imeanzisha mpango maalumu wa kuimarisha mchezo wa kuogelea nchini kwa kumwalika kocha wa kimataifa, Ben Lee kutoka Marekani, mwenye uzoefu wa kufundisha katika kiwango cha NCAA na Olimpiki.

Amesema lengo la ujio wa kocha huyo ni kuinua kiwango cha waogeleaji wa Tanzania na kuifanya nchi kuwa kitovu cha mchezo wa kuogelea Afrika Mashariki.

Akizungumza na waandishi wa habari, Fatma, amesema hatua hiyo inakuja wakati Tanzania ikijiandaa kushiriki mashindano mbalimbali ya kimataifa, ikiwemo CANA Zone 3, ambapo takribani waogeleaji 40 wanatarajiwa kushiriki.

Ameeleza kuwa uzoefu wa Ben Lee utasaidia kuongeza uwezo wa waogeleaji wa Tanzania pamoja na kuwajengea makocha mbinu za kisasa za kufundisha.

Amesema mafunzo hayo yamegawanywa katika makundi matatu ambayo ni mafunzo kwa makocha, wazazi na waogeleaji wenyewe ili kuongeza uelewa wa mchezo huo kwa wadau wote. Mafunzo ya makocha yataanza Julai 28 hadi Julai 30, yakifuatiwa na ngazi ya Beginner kuanzia Julai 30 hadi Agosti 1, Intermediate kuanzia Agosti 3 hadi 7, na Advanced kuanzia Agosti 10 hadi 14.

Fatma amesisitiza kuwa mafunzo kwa makocha yatatolewa bila malipo, licha ya gharama za kumleta kocha huyo kubebwa na Monti International School. Amesema makocha wote wenye usajili wa Tanzania Swimming Association wanakaribishwa kushiriki ili kupata maarifa yatakayosaidia kuinua kiwango cha mchezo wa kuogelea nchini. Mafunzo yote yatafanyika Monti International School, Mikocheni, kuanzia saa mbili hadi saa tano asubuhi kila siku.

Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Ufundi Chama Cha Kuogelea Amina Mfaume Chama amesema ni maendeleo ya mchezo wa kuogelea Tanzania na kuongeza uwezo wa kuogelea nchini.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button