Mabingwa mbio za baiskeli kufanyika Agosti 30

DAR ES SALAAM: CHAMA cha Baiskeli Mkoa wa Dar es Salaam (CHABADA), kimeandaa mashindano ya mkoa Agosti 30, 2026, ikiwa ni hatua ya kutafuta mabingwa watakaowakilisha mashindano ya Taifa yatakayofanyika Dodoma Septemba 12 na 13 mwaka huu.
Mashindano hayo yanatarajiwa kukutanisha waendesha baiskeli kutoka wilaya zote tano za Dar es Salaam, huku chama hicho kikisema ushindani huo ni muhimu kuibua na kuandaa wachezaji watakaoiwakilisha Dar es Salaam kwenye mashindano ya Taifa.
Mwenyekiti wa Chabada, Husseni Ali, amesema kwa muda mrefu mkoa huo haujaandaa mashindano ya kupata bingwa wa mkoa, hivyo wameamua kuyarejesha ili kutoa nafasi kwa waendesha baiskeli kujipima uwezo.
Amesema waendesha baiskeli wanaume watashindana umbali wa kilometa 69, wakati wanawake watashindana kilometa 50., hivyo kuwaomba waendesha baiskeli Dar kujitokeza kushiriki.



