‘Hakuja ujuzi bila mwalimu’

SONGEA: Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Carolyne Naomba, amesema hakuna taaluma inayoweza kujengwa bila msaada wa mwalimu.
Profesa Naomba amesema hayo jana, alipokutana na walimu tarajali katika Chuo cha Ualimu Songea, mkoani Ruvuma .
“Hakuna mtu anayeweza kuwa na ujuzi bila kupitia mikononi mwa mwalimu,” alisema.
Alisema kuwa madaktari, wahandisi, viongozi na wataalamu wa kada mbalimbali walifundishwa na walimu katika hatua fulani ya maisha yao.
Alisisitiza kuwa serikali inaendelea kuinua hadhi ya ualimu kupitia maboresho ya mitaala ya mafunzo, kuongeza viwango vya sifa za kujiunga na taaluma hiyo na kuboresha mazingira ya kazi.
Hatua hizo zinaendana na utekelezaji wa mtaala mpya, huku Serikali ikisisitiza kuwa ubora wa elimu hauwezi kutenganishwa na ubora wa mwalimu.
Prof. Nombo amesisitiza kuwa mwalimu si mtoa maarifa pekee, bali ni mlezi wa maadili na mjenzi wa kizazi kinachobeba mustakabali wa taifa.



