Songwe yaongoza njia mageuzi ya kiuchumi Dira 2050

SONGWE: Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo amesema Mkoa wa Songwe unapaswa kutazamwa kipekee utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050 kwa kujenga uchumi unaozalisha fursa, ajira.

Akizungumza katika siku ya kwanza ya Jukwaa la Dira 2050 mkoani Songwe, Prof Mkumbo amesema lengo ni kuubadilisha mkoa kutoka kuwa wa kiutawala na kuwa mkoa wa kiuchumi, kwa kuanzia kwenye fursa, kwenda kwenye uwekezaji, uzalishaji, kuongeza thamani na hatimaye mauzo ya nje.

Akizungumza katika Jukwaa la Dira 2050 katika Mkoa wa Songwe, lililoandaliwa na Mkuu wa Mkoa huo, Jabiri Makame, Prof Mkumbo amesema atahakikisha anapita kila mkoa kuzileta pamoja sekta ya umma na binafsi kwa lengo la kutekelezaji wa Dira 2050.

Amesema wabebaji wakubwa wa maono katika Dira ya 2050 ni sekta binafsi, hivyo ushiriki wao kwenye jukwaa hilo umekuwa wenye tija.

Prof Mkumbo pia amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Songwe kwa kuandaa jukwaa la Dira 2050, sambamba na kushirikisha sekta binafsi kwenye jukwaa hilo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Jabari Makame amesema mkoa huo una fursa nyingi za kilimo, madini, kijografia na biashara.

Pia amehamasisha ushirikiano kati ya Sekta ya Umma na Binafsi katika kuyafikia maono ya Dira 2050.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button