• Kuhusu HabariLEO
  • Matangazo: Maelekezo & Bei
  • Nunua E-Paper
HabariLeo
No Result
View All Result
No Result
View All Result
HabariLeo
No Result
View All Result

Wakimbiaji zaidi ya 1,200 kushiriki Mbio kubwa za Ruaha

Na Frank Leonard by Na Frank Leonard
April 28, 2026
in Michezo na Burudani
1
Wakimbiaji zaidi ya 1,200 kushiriki Mbio kubwa za Ruaha

IRINGA: Zaidi ya wakimbiaji 1,200 kutoka ndani na nje ya nchi wanatarajiwa kushiriki Great Ruaha Marathon Season Five itakayofanyika Julai 3 na 4 mwaka huu mkoani Iringa, huku Mwigulu Nchemba akitarajiwa kuwa mgeni rasmi katika tukio hilo kubwa la kimichezo na kitalii.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, amezindua rasmi maandalizi ya mbio hizo maarufu kwa jina la Great Ruaha Marathon Vibe Kitalii Season Five, akieleza kuwa imeendelea kuwa nyenzo muhimu ya kukuza utalii, michezo na uchumi wa wananchi wa mkoa huo.

Uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali, wadau wa utalii, wanamichezo pamoja na waandishi wa habari, huku ukionesha mwitikio mkubwa kutoka kwa jamii na sekta mbalimbali.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa alisema mashindano ya mwaka huu yataendelea kuitangaza Iringa na vivutio vyake vya kipekee ndani na nje ya nchi, sambamba na kuleta fursa mpya za kiuchumi kwa wananchi.

Alisema Serikali imeendelea kuboresha miundombinu ya utalii mkoani Iringa ikiwemo barabara ya Iringa–Msembe pamoja na uboreshaji wa Uwanja wa Ndege Iringa hatua inayochochea utalii na biashara zinazohusiana.

RC James alisisitiza kuwa mbio hizo si tukio la michezo pekee, bali ni jukwaa pana la maendeleo linalounganisha sekta za utalii, uhifadhi wa mazingira, afya, michezo na uchumi wa jamii.

Aliwahimiza wananchi kuchangamkia fursa zitokanazo na tukio hilo kupitia huduma za malazi, usafiri, biashara ndogondogo na huduma nyingine, huku akisisitiza umuhimu wa kulinda mazingira na vyanzo vya maji vya Mto Great Ruaha Mkuu.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), July Lyimo, alisema mashindano hayo yamekuwa na mchango mkubwa katika kukuza utalii wa ndani na nje ya nchi, hususan ukanda wa Kusini mwa Tanzania.

Alisema Hifadhi ya Taifa ya Ruaha inaendelea kujitangaza kimataifa sambamba na juhudi za Serikali chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kupitia kampeni ya The Royal Tour, huku TANAPA ikilenga kufikia watalii milioni nane ifikapo mwaka 2030.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la Sustainable Youth Development Partnership (SYDP) linaloratibu mbio hizo, Edward Athanas Milinga, alisema katika misimu minne iliyopita mbio hizo zimeleta mafanikio makubwa ikiwemo kuongezeka kwa mwamko wa utalii, kuimarika kwa juhudi za uhifadhi kupitia ushirikishwaji wa jamii pamoja na kukuza vipaji vya riadha kwa vijana.

Aliongeza kuwa tukio hilo limefungua fursa nyingi za kiuchumi na kijamii kwa wafanyabiashara, vijana na wananchi kwa ujumla, huku akiomba ushirikiano zaidi katika uhamasishaji na ushiriki wa taasisi mbalimbali.

Awali, Mratibu wa mbio hizo, Hamimu Kilahama, alisema msimu huu wa tano unalenga kupanua mafanikio ya misimu iliyopita kwa kuongeza ushiriki wa kimataifa na kukuza zaidi tasnia ya utalii kupitia michezo.

Uzinduzi wa Great Ruaha Marathon Season Five unaashiria hatua mpya ya maandalizi ya tukio hilo kubwa la kimichezo na kitalii, linaloendelea kuimarisha nafasi ya Iringa kama kitovu cha utalii na michezo nchini Tanzania.

Previous Post

Utekelezaji hafifu wa Sera watajwa chanzo cha ukatili kijinsia

Next Post

Dk Kijaji awasili Zimbabwe kushiriki mkutano wa utalii

Next Post
Dk Kijaji awasili Zimbabwe kushiriki mkutano wa utalii

Dk Kijaji awasili Zimbabwe kushiriki mkutano wa utalii

Comments 1

  1. istanbul kentsel dönüşüm says:
    3 weeks ago

    Her değişim sürecinde nedense hep teknik detaylara boğuluyoruz. Bizim ysgrup projelerinde edindiğimiz en büyük tecrübe, insan faktörünü ilk sıraya koymadığınızda o planların kağıt üstünde kalması oldu. [dsppvtebjlnynsjjnp]

    Reply

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Zilizosomwa Ziadi

  • Mradi mpya kupunguza msongamano bandari ya Dar
    Mradi mpya kupunguza msongamano bandari ya Dar
  • Kairuki apongeza upanuzi  huduma za intaneti
    Kairuki apongeza upanuzi huduma za intaneti
  • Mbegu bora, chachu ya kilimo cha ushindani
    Mbegu bora, chachu ya kilimo cha ushindani
  • Luizer ampongeza Asha Baraka
    Luizer ampongeza Asha Baraka
  • Luizer awasihi wanawake kutunza ngozi
    Luizer awasihi wanawake kutunza ngozi

Latest on this theme

  • (no title)
    by Yohana Shida, Geita
    September 5, 2022
  • (no title)
    by NEW YORK, Marekani
    September 6, 2022

  • Kuhusu HabariLEO
  • Matangazo: Maelekezo & Bei
  • Nunua E-Paper

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

No Result
View All Result

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.