Samia kutunukiwa shahada ya heshima Nigeria

DODOMA — Rais Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kutunukiwa shahada ya heshima na Chuo Kikuu cha Nasarawa nchini Nigeria kupitia njia ya mtandao.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, tukio hilo litafanyika Aprili 11, 2026 saa 7:00 mchana katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, na litakuwa likirushwa mubashara kupitia televisheni na mitandao ya kijamii.
Kutunukiwa kwa shahada hiyo kunatambua mchango wa Rais Samia katika uongozi, maendeleo na ushirikiano wa kimataifa.



