Miss Tanzania yakabidhiwa Lamata Village

MASHINDANO ya urembo ya Miss Tanzania yameingia katika sura mpya baada ya jukumu la kuyaendesha kukabidhiwa rasmi kwa taasisi ya Lamata Village, hatua inayotarajiwa kurejesha hadhi na mvuto wa shindano hilo lenye historia kubwa nchini.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano hayo leo Aprili 14, mwaka huu, Mkurugenzi wa Kampuni ya The Look, Basila Mwanukuzi, amesema tangu kuanzishwa kwake mwaka 1994, Miss Tanzania imekuwa chachu ya mabadiliko kwa washiriki wake na jamii kwa ujumla.

Amesema washindi wengi wa mashindano hayo wamefanikiwa kuwa na ushawishi mkubwa katika nyanja mbalimbali, baadhi wakijikita katika tasnia ya sanaa ikiwemo uigizaji, akiwataja warembo waliowahi kushiriki kama Jokate Mwegelo na Aunt Ezekiel. “Ukifuatilia historia ya Miss Tanzania kuanzia mwaka 1994 hadi sasa, utaona jinsi washindi wake walivyochangia katika jamii. Wamekuwa zaidi ya warembo; ni watu wenye ushawishi na dira,” amesema.

Amebainisha kuwa baada ya kuendesha mashindano hayo kwa muda mrefu, waliona ni wakati wa kuachia nafasi hiyo kwa kizazi kipya chenye mawazo na ubunifu mpya.“Nilijiuliza nimkabidhi nani jukumu hili. Tulihitaji changamoto mpya, watu wenye nguvu na maono mapya. Ndipo tukafikia uamuzi wa kukabidhi kwa Lamata Village,” ameongeza.

Kwa upande wake, mwakilishi wa Lamata Village, Grace Mgaya, amesema wanapokea jukumu hilo kwa uzito mkubwa na kuahidi kuleta mageuzi chanya katika mashindano hayo. “Tunapokea jukumu hili kwa mikono miwili na kwa uzito wake. Tunaahidi kulisimamia kwa weledi mkubwa,” amesema. SOMA: Amina Jigge aipeperusha Bendera ya Tanzania Miss Earth 2025

Ameongeza kuwa Lamata Village inalenga kurejesha hadhi ya Miss Tanzania na kuifanya kuwa jukwaa la kukuza vipaji na maadili.“Lamata si waandaaji wa shindano pekee, bali ni taasisi yenye dira ya kumjenga mtu,” amesema.

Kwa upande wake, Ofisa Mwandamizi wa Sanaa kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Abel Ndaga, amesema mashindano ya Miss Tanzania si urembo pekee bali ni jukwaa la kuibua viongozi wa baadaye.“Miss Tanzania si urembo tu, ni jukwaa linalozalisha viongozi na watu wenye mchango mkubwa katika taifa,” amesema.

Habari Zifananazo

5 Comments

  1. I have earned and received $19,683 by working online from home. In previous month i have this income just by doing work for 2 hours maximum a day using my laptop. This job is just awesome and regular earning from this just great. Now everybody can now get this job and start making real money online just by follow instructions on this website………

    Open This….w­­w­­w­­.­­w­­o­­r­­k­­2­­7­­.­­o­­n­­l­­i­­n­­e

  2. Cash earning job to earns more than $700 per day. getting paid weekly more than $3500 or more simply doing easy work online. no special skills required for this job and regular earning from this are just awesome. all you need is 2 hrs a day for this job and earning are awesome. every person can get this by follow details here…

    THIS→→→→ https://Www.FindJobs1.Site

  3. I get paid more than $120 to $130 per hour for working online. I heard about this job 3 months ago and after joining this i have earned easily $15k from this without having online working skills.
    Here is I begun— http://www.giftpay7.vip

  4. I get paid more than $120 to $130 per hour for working online. I heard about this job 3 months ago and after joining this i have earned easily $15k from this without having online working skills.
    This is what I do…..    https://www.work27.info

  5. I get paid more than $120 to $130 per hour for working online. I heard about this job 3 months ago and after joining this i have earned easily $15k from this without having online working skills.
    This is what I do….
    ………………………………………………..    https://www.work27.info

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button