Ajali yaua watano Morogoro

WATU Watano wamefariki dunia eneo la Mikumi, wilayani Kilosa, mkoani Morogoro katika ajali iliyohusisha gari ndogo yenye namba za usajili IT 6954 DNN, kugongana uso kwa uso na gari kubwa la mafuta lenye namba za usajili RL 2686.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Fortunatus Musilim, ajali hiyo ilitokea usiku wa kuamkia Desemba 26, 2022 na kwamba gari ndogo ilikuwa ikitokea Dar es Salaam kuelekea Tunduma, wakati gari kubwa lilikuwa likitokea Iringa kuelekea Morogoro, huku chanzo cha ajali kikitajwa ni uzembe wa dereva wa gari ndogo.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button