Vijana wapewa mbinu kujikwamua kiuchumi

MWENYEKITI wa Bodi ya Uwekezaji  ya UTT AMIS, Profesa Faustine Kamuzora amewashauri vijana ambao ni kundi kubwa na wenye nguvu ya kufanya kazi wawekeze kwenye mfuko huo ili wapate mtaji wa kujinyanyua kibiashara na kiuchumi katika maisha yao.

Profesa Kamuzora amesema  hayo  leo  wilayani Kahama mkoani Shinyanga kwenye kufungua kituo cha uwekezaji UTT AMIS huku akieleza wakiwekeza takribani miaka mitatu watakuwa wamekuza mitaji yao na kuondokana na wimbi la umaskini huku ikiendeleza dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025 hadi 2050.

Profesa Kamuzora amesema vijana hawana budi kuwekeza  kwani  watu wengi wamekuwa masikini kwa kukosa  elimu ya fedha hivyo wanapaswa wajibidishe  na kuwekeza ili waweze kufaidika na kusaidia ndugu zao.

“Mnaweza kuweka fedha  kidogo kidogo  hasa vijana mtaweza kunufaika kwani shughuli mnazofanya za uchimbaji wa madini ,biashara na kilimo ni fursa kwenu kuwekeza sasa”amesema Profesa Kamuzora.

Mkurugenzi Mtendaji wa Uwekezaji UTT AMIS  Simon Migangala amesema walianzs mwaka 2005 na asset ya shilingi bilioni moja na sass ni miaka 20  wameenda wakikuwa na kufikia asset ya shilingi bilioni 20  ambapo kila mwaka asset ilikuwa bilioni moja moja huku akieleza sababu za kukua kwao ni kujiamini na kuwepo uaminifu.

“Tunipongeza serikali kwa kuendelea kutuwezesha mazingira mazuri  ya uwekezaji  na kuwa bora kazi iliyobaki ni kuhudumia wananchi kuhakikisha wanawekeza na kupata faida kwa wakazi wa Kahama na Mikoa ya jirani,”alisema Migangala.

Migangala amesema sehemu kubwa huduma inapatikana zaidi kwenye mitandao na zinaendelea kuboreshwa  kupitia tecknolojia na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu imeonekana kukuza uwekezaji nchini.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Frank  Nkinda amesema  tathimni iliyofanyika na kufungua kituo hiki imethihirisha kupanua wigo na kuwawezesha wananchi kupata elimu ya fedha na kuweka akiba.

Nkinda amewapongeza kwa kiasi cha rasilimali walichowekeza  Sh trilioni 3.5 kwa wawekezaji 500,000 hivyo matumaini  yaliyopo kwa ujio huo ni kuongeza ukuaji wa kiuchumi kwa wananchi wa wilaya hii.

“Serikali  ipo sambamba na taasisi za kifedha kwa mujibu wa kisera  itachochea  na kuleta hamasa kwa  wananchi wa mjini na vijijini  ninawaomba kwenye mkutano na wachimbaji wadogo muwepo mtoe elimu hii waweze kuwekeza,”amesema Nkinda.

Baadhi ya wananchi walio hudhuria ufunguzi huo Herieth John na Daud James wamesema uwekezaji huo ni mzuri utawafanya kuinuka zaidi katika biashara zao na kusomesha watoto.

 

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button