Handeni Mji yaweka mikakati kuimarisha afua za lishe

TANGA: HALMASHAURI ya Mji Handeni imeainisha mikakati mitano ya kuimarisha utekelezaji wa afua za lishe, ili kukabiliana na changamoto za utapiamlo na kupunguza idadi ya watoto wanaozaliwa wakiwa na uzito pungufu.
Akisoma taarifa ya Tathmini ya Utekelezaji wa Afua za Lishe kwa Robo ya Kwanza, Novemba 11, 2025, Ofisa Lishe wa Halmashauri hiyo, Ester Herman, amesema mikakati hiyo inalenga kuongeza uelewa wa jamii kuhusu lishe bora na kuhakikisha huduma muhimu za lishe zinatolewa kikamilifu katika ngazi zote.
Ametaja baadhi ya mikakati hiyo kuwa ni kuhamasisha jamii kuhakikisha watoto chini ya miaka mitano wanaendelea kuhudhuria kliniki hata baada ya kukamilisha chanjo, na kushirikiana na idara za elimu msingi, sekondari pamoja na kamati za lishe za kata kuhamasisha wazazi kuchangia huduma za chakula shuleni.
Aidha, amesema halmashauri imejipanga kuhimiza wajawazito kufika mapema kwenye vituo vya afya, ili kupunguza idadi ya watoto wanaozaliwa wakiwa na uzito pungufu, sambamba na kushirikiana na Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kutoa elimu ya kilimo na ufugaji bora wa kuku, bata na sungura ili kuongeza upatikanaji wa chakula chenye virutubisho.

Ester ameongeza kuwa halmashauri pia itashirikiana na sekta mtambuka katika maadhimisho ya siku ya afya na lishe ngazi ya mtaa, kama njia ya kuhamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika masuala ya lishe.
Hata hivyo, amebainisha kuwepo kwa changamoto kadhaa zinazohitaji ufuatiliaji wa karibu, ikiwemo baadhi ya wazazi kuchelewa kuwapeleka watoto wenye utapiamlo mkali vituoni kutokana na imani za kishirikina, na mahudhurio hafifu ya kliniki baada ya watoto kukamilisha ratiba ya chanjo.




I make up to $90 an hour working from my home. My story is that I quit working at Walmart to work online and with a little effort I easily bring in around $40h to $86h… Someone was good to me by sharing this link with me, so now i am hoping i could help someone else out there by sharing this link…
Try it, you won’t regret it!….. https://www.job40.media
I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
.
HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us →→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com