Samia aunda Tume huru ya uchunguzi wa matukio ya uchaguzi

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa mamlaka aliyonayo chini ya kifungu cha 3 cha Sheria ya Tume ya Uchunguzi, Sura ya 32, ameunda Tume huru ya uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea nchini wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 29 mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa mjini Dodoma na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka, Rais Samia pia amemteua Jaji Mkuu Mstaafu wa Mahakama ya Tanzania, Mohammed Chande Othman, kuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo. SOMA: Rais atangaza Baraza la Mawaziri la kimkakati

Wajumbe wengine walioteuliwa ni  Jaji Mkuu Mstaafu wa Mahakama ya Tanzania Profesa Ibrahimu Khamis,Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu  Balozi Ombeni Sefue , Balozi  Radhia Msuya, Balozi Gen.  Paul Meela ,IGP Mstaafu Said Mwema , Balozi David Kapya na Aliyewahi kuwa Katibu Mtendaji ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika.

 

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button