Mwakagenda Mwenyekiti mpya Halmashauri Rungwe

MBEYA; MADIWANI katika Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe wamemchagua Gabriel Mwakagenda kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM) kuwa Mwenyekiti wa halmashauri hiyo.

Katika Kikao cha kwanza cha Baraza la Madiwani kilichofanyika leo Mwakagenda amechaguliwa kwa kupata kura za ndiyo zote  42 zilizopigwa.

Akizungumza mara baada ya kuchaguliwa Mwakagenda ameahidi  ushirikiano kwa madiwani wote akiwemo Diwani wa Kata ya Makandana wa Chama cha ACT-Wazalendo akisema kitendo cha yeye kuungana na madiwani wa CCM  kunamaanisha ana lengo la kuwa na umoja katika kuwaletea maendeleo wananchi.

 

 

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button