CCM kuifanya hospitali ya Mkapa kuwa ya kimataifa

MOROGORO: Mgombea Mwenza wa Urais kupitia CCM, Dk. Emmanuel Nchimbi, amesema Serikali ya CCM imepanga kuibadilisha Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma kuwa kituo bora cha kimataifa cha mafunzo, huduma za kibingwa na utafiti wa kitabibu katika miaka mitano ijayo endapo itapata ridhaa ya kuendelea kuongoza nchi.

Akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika Nkuhungu jijini Dodoma, Dk. Nchimbi alisema hospitali hiyo itawezesha kufundisha madaktari, wauguzi na wataalamu wa afya kutoka ndani na nje ya nchi, sambamba na kuongeza huduma za kibingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.

Aidha, akizungumzia sekta ya nishati, Dk. Nchimbi alisema uongozi wa Rais Samia umefanya mageuzi makubwa, ikiwemo kukamilisha ufungaji wa mitambo katika Bwawa la Mwalimu Nyerere na kuongeza uzalishaji wa umeme kutoka megawati 1,602 hadi 3,078, pamoja na kufikisha umeme katika vijiji vyote 12,318 vya Tanzania.

Alitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi Oktoba 29 kumpa kura Rais Dk. Samia pamoja na wagombea wa ubunge na udiwani wa CCM ili kazi ya maendeleo iendelee.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. I’m making over $25,000 a month working part-time. I kept hearing other people talk about how much money they were making online, so I decided to look into it. Well, it’s all true and has completely changed my life. This is what I do. Check it out by visiting the following link:

    COPY THIS →→→→ http://Www.Work99.Site

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button