Kamati ya bunge yaipa  5 serikali

SONGEA: Kamati ya Kudumu ya Bunge Utawala , Katiba na Sheria imeipongeza serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka fedha  katika miradi yenye tija Kwa  watu kupitia mfuko wa TASAF.
Kamati imetoa pongezi hizo baada ya kukagua mradi wa Stendi ya Mabasi Peramiho na soko la bidhaa mbalimbali, Madaba.
Akizungumza mbele ya wananchi Mwenyekiti wa Kamati hiyo  Dk Joseph Mhagama  aliishukuru  serikali kwa miradi hiyo .
Awali,  Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais   Ridhiwani Kikwete alimshukuru Rais  Samia  kwa kuwezesha fedha kiasi cha Sh. Bilioni 1.5  kutekeleza miradi mbalimbali katika Mkoa wa Ruvuma pekee kupitia TASAF.