Makonda aahidi neema kwa vijana

ARUSHA: MGOMBEA ubunge Jimbo la Arusha Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Paul Makonda amesema wananchi wakimchagua atahakikisha vijana wanapatiwa mikopo na fursa mbalimbali.

Aidha, lengo ni vijana hao kujikwamua kiuchumi ili waweze kujiajiri na kuachana na matukio ya uhalifu.

Makonda alisema hayo Oktoba 26 alipokuwa akipita mtaa kwa mtaa kuhamasisha wananchi kupiga kura Oktoba 29,mwaka huu.

Alisema anatambua kuwa wapo baadhi ya vijana wanaofanya matukio ya uharifu kwa sababu ya ugumu wa maisha, hivyo katika uongozi wake atawawezesha vijana kiuchumi vijana ili wafanye majukumu vizuri kwa kuibua fursa za kiuchumi ili kila vijana wawe na shughuli za kufanya.

“Usalama wa nchi ni jukumu la wananchi wote kuhakikisha maeneo wanayoishi yanakuwa salama,watoto wanafanya matukio ni watoto wetu kila mmoja anatakiwa kuwa sehemu ya ulinzi wa watoto kuanzia ngazi za familia,”alisema Makonda.

Aliahidi kuongeza thamani ya mabalozi na ngazi za mashina inarejeshwa, ili wawe walinzi wa ulinzi na usalama katika maeneo yao chini ya usimamizi wa wenyeviti wa serikali za mitaa na vijiji ili kila kaya iwe salama.

“Ndani ya halmashauri kuna aina nne za mikopo inayotokana na makusanyo ya mapato ya ndani inayotolewa kwa wanawake, vijana na makundi kupitia ofisi mbalimbali za serikali kama Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum na Ofisi ya Waziri Mkuu ili kuwawezeshaji kiuchumi vijana kiuchumi nao waondokane na ukosefu wa ajira na wananchi wanaelewa taratibu za mikopo hiyo na kuipata kwa urahisi,”alisema.

Makonda alisema Tanzania bado haijafikia kiwango cha uzalishaji wa kutosha kwa sababu gesi nyingi zinaagizwa kutoka nje ya nchi, huku matumizi yake yakiongezeka zaidi ya uzalishaji wa ndani.

Alisema jimbo hilo bado lipo nyuma katika miundombinu ya barabara, hivyo atahakikisha miundombinu hiyo inaboreshwa ili kurahisisha shughuli za kiuchumi na kijamii kwa wananchi.

Aidha,aliwaomba wananchi kujitokeza kupiga kura ili wasipoteze haki yao ya msingi kwa sababu maamuzi watakayoyafanya ndio yataamua uelekeo wa taifa katika kipindi cha miaka mitano.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..

    .

    This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button