Mgombea urais Makini aahidi pareto Kilimanjaro

KILIMANJARO; MGOMBEA urais kupitia Chama cha Makini, Coaster Kibonde amesema serikali ya chama hicho itaanzisha kilimo cha pareto Mkoa wa Kilimanjaro ili kuimarisha uchumi wa mkoa huo.

Kibonde alisema hayo wakati wa mkutano wa kampeni katika viwanja vya soko la Manyema, Manispaa ya Moshi mkoani humo juzi.

“Utafiti uliofanywa na wataalamu wa chama chetu umebaini kuwa zao la pareto ambalo nalo ni muhimu katika kukuza uchumi kutokana na kuwa na soko kubwa maeneo mbalimbali duniani kote linaweza kustawi mkoani Kilimanjaro,” alisema.

Aliongeza: “Kahawa ndiyo lilikuwa zao muhimu kiuchumi lakini kwa sasa limeshuka kutokana na sababu mbalimbali, njia ya kuimarisha uchumi wenu na wa mkoa kwa ujumla ni kuanzisha kilimo cha zao lingine”.

Akizungumzia zaidi kuhusu kilimo, Kibonde alisema serikali yake itaboresha viwanja vya ndege katika mikoa yote ili kurahisisha mauzo ya mazao yanayozalishwa nchini.

“Viwanja hivi vikiwa bora, wakulima watakuwa na uwezo wa kusafirisha mazao yao kwa urahisi badala ya kutegemea uwanja wa ndege wa Julius Nyerere (Kiwanja cha Kimataifa cha Ndege cha Julius Nyerere-JNIA) na ule wa KIA (Kilimanjaro International Airport)” alisema Kibonde.

Aliongeza: “Kuna wafanyabiashara wa nje ambao wanapenda kuja kununua mazao moja kwa moja hapa nchini, hawa nao watanufaika maana watakuwa wanashukia kwenye uwanja ulioko eneo analokwenda kununua mazao ya kilimo badala ya kushukia Kilimanjaro au Dar es Salaam na kisha kuanza safari ya kwenda maeneo yaliko mazao anayotaka kununua.”

Kwa upande wa elimu, Kibonde alisema serikali ya Makini itaanzisha mpango wa kugharimia elimu ya juu kwa wanafunzi wanaokwenda kusoma nje ya nchi.

“Serikali itakayoongozwa na Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Makini itahakikisha inagharamia wanafunzi wote wanaokwenda kusoma nje ya nchi; haitakuwa ni mikopo kwao bali ni kwa ajili yao ili wapate elimu nzuri waje kuliongoza taifa baadaye”, alisema.

Kibonde pia alisema katika sekta hiyo ya elimu, baada ya kuapishwa kuwa rais atapandisha mishahara ya walimu.

“Hawa ndio watu muhimu kabisa katika taifa letu maana hakuna aliyefika hapa tulipo sasa hivi kila mtu na fani yake ambaye hakupitia kwa Mwalimu,” alisema.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..

    .

    This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button