Msitu wa Ngezi; thamani itakayoipaisha Pemba

PEMBA ni moja ya visiwa vikongwe vya Zanzibar kinachoishi chini ya kivuli cha kisiwa dada chenye harakati nyingi cha Unguja. Kisiwa hicho tulivu, chenye kijani kibichi, kwa kiasi kikubwa hakijapata watalii wengi wanaokitembelea, lakini kama upepo unavyovuma katika Visiwa vya Zanzibar ndivyo hadithi ya kisiwa hicho itakavyobadilika haraka.
Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi ametangaza kuwa serikali yake ‘itageuza kila jiwe’ kuhakikisha inafungua fursa zote za utalii Pemba ili kuongeza watalii kila mwaka kutoka takribani 200,000 hadi zaidi ya wageni 400,000 katika miaka mitatu ijayo. Lengo la kitaifa (kwa Zanzibar) ni kuongeza watalii kutoka zaidi ya watalii 700,000 wa sasa hadi milioni moja ifikapo mwakani.
Katikati ya mageuzi hayo kuna mchanganyiko wa asili usiopatikana popote Afrika Mashariki; huo ni Hifadhi ya Msitu wa Ngezi ambayo ni moja ya maeneo muhimu ya msitu wa asili na ufukwe wa Vumawimbi uliobarikiwa mchanga safi mweupe unaokutana pamoja kutengenza mandhari ya kuvutia.
Kwa pamoja vitu hivyo vinatengeneza ukanda wa utalii ambao upande mmoja ni hazina ya ikolojia, upande mwingine ni hifadhi ya utamaduni na sehemu nyingine ni injini ya uchumi kwa wajasiriamali wadogo wa kisiwa hicho. Himaya ya vito vya zamaradi Kuingia kwenye Msitu wa Ngezi ni kama kuingia katika ulimwengu uliohifadhiwa kwa kioo.

Ni kama mwavuli mkubwa ulioinama juu, ukichuja mwanga wa jua kuwa kijani kibichi na dhahabu vikichagizwa na mwangwi wa sauti za ndege kutoka pande zote pamoja na harufu ya karafuu mwitu na miti ya karne nyingi inayoning’inia hewani.
Katibu Mkuu Wizara ya Utalii na Malikale, Dk Aboud Suleiman Jumbe anasema: “Msitu huu si tu urithi wa Pemba, ni faida yetu ya ushindani…”Anaongeza: “Ngezi ni moja ya misitu ya asili iliyosalia katika visiwa vyetu. Tukiihifadhi vyema na kuiingiza katika utalii endelevu, inaweza kubadilisha sana maisha yetu.”
Bioanuwai ya Ngezi hailinganishwi na mahali popote Zanzibar. Kutembea kwenye njia zake nyembamba za asili, kukutana na maua mazuri na adimu, jongoo wakubwa na aina za ndege wasiopatikana kwingine ni jambo linalofurahisha na kuvutia Msitu wa Ngezi; thamani itakayoipaisha Pemba wanaofanikiwa kufika hapo.
Waongoza watalii wa ndani, wengi wao wakiwa ni wataalamu wa mambo ya asili waliojifunza wenyewe, wameboresha ujuzi katika kutafuta riziki zao, wakitoa ofa za matembezi ya kuona ndege alfajiri, ziara za mikoko, na safari za usiku kwa wale wanaotaka kujua kuhusu maisha ya wakazi wa Pemba usiku.
Dk Jumbe anasisitiza kuwa, uhifadhi unasalia kuwa kanuni elekezi; “Utalii una maana ikiwa tu asili inaendelea kuwepo. Sera zetu zinahakikisha kwamba Ngezi na Vumawimbi zinasalia kuwa safi kwa vizazi vijavyo.”

Asili inanong’ona Mwongoza watalii kisiwani humo, Khalid Kombo Khamis anasema Pemba bado ni tajiri katika utamaduni uliotunzwa vizuri, ikiwa na zaidi ya maeneo 45 ya kihistoria yaliyotangazwa kwenye gazeti la serikali. “Serikali imejizatiti kikamilifu kutangaza utalii Pemba ikiwa ni pamoja na utalii wa kijamii na utalii kwa wote. Lengo letu ni kuhakikisha sekta ya utalii inamnufaisha kila mtu,” anasema.
Anasema nje kidogo ya ukingo wa Kaskazini wa msitu huo kuna ufukwe wa Vumawimbi, wenye mchanga mweupe na maji safi ya bluu kijani. Anasema maeneo hayo bado hayakumbwa na uharibifu na kwa kiasi kikubwa hayajaendelezwa huku akiongeza kuwa ni moja ya maeneo yanayoonekana kupitwa na wakati.
Watalii wanaosafiri kuelekea Kaskazini mara nyingi huelezea uzuri wa eneo hilo kuwa ni mojawapo ya fukwe bora zaidi walizowahi kuona. Mmoja wa wageni kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu, Ahmed Mohammed anasema, “Nilikuja msituni.
Nilikaa kwenye ufukwe huu (Vumawimbi). Ni amani ya ajabu, kama vile asili inavyonong’ona.” Pamoja na maji tulivu yanayofaa kuogelea, kutoa fursa ya matembezi ya familia, tafrija za ufukweni na kutoa nafasi ya kutafakari kwa utulivu. Anasema Vumawimbi inatoa utulivu usiopatikana kirahisi katika maeneo ya kisasa ya utalii. Vijana katika hadithi ya Ngezi Kuinuka kwa Ngezi si tu hadithi ya kiikolojia, bali pia hadithi ya mwanadamu.
Kando ya msitu, vijana wa eneo hilo “ Serikali imejizatiti kikamilifu kutangaza utalii Pemba ikiwa ni pamoja na utalii wa kijamii na utalii kwa wote. Lengo letu ni kuhakikisha sekta ya utalii inamnufaisha kila mtu,” katika idadi inayoongezeka wameunda biashara ndogo zinazohudumia wageni.

Huduma hizo ni pamoja na kukodisha baiskeli, kuuza bidhaa zilizotengenezwa kwa mikono, ziara za kuongoza watalii, kukodisha vifaa vya kupiga kambi, kupika vyakula vya asili, huduma za kupiga picha za asili na hata safari fupi za baharini. “Tulikuwa tukija hapa kwa ajili ya kuni au uvuvi tu,” anasema mwongoza watalii Shaaban Juma Hassan (26), mmoja wa vijana wanaofanya kazi katika utalii wa mazingira katika eneo hilo. “Sasa ninaweza kupata riziki kwa kulinda msitu huu.
Watalii wanataka kujifunza kutoka kwetu, na hilo linatufanya tujivunie.” Baadhi wameunda vyama vya ushirika ili kukusanya mapato na kuwekeza katika mafunzo, huduma ya kwanza na utunzaji wa mazingira. ZIPA inafungua mlango wa uwekezaji mpya Nyuma ya pazia, Mamlaka ya Kukuza Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA) inaweka mazingira ya kuwavuta wawekezaji katika sekta ya miundombinu ya utalii.
Mkurugenzi Mtendaji wa ZIPA, Saleh Saad Mohamed anaamini kuwa ‘wakati wa dhahabu’ kwa Pemba umewadia; “Tuna nafasi ya kufanya utalii kwa njia tofauti hapa,” anasema. “Tunakaribisha wawekezaji ambao wataheshimu asili, watashirikiana na jamii na kuleta thamani ya muda mrefu Pemba.” “Malazi, nyumba za kulala wageni, migahawa, shughuli za baharini, kuna nafasi ya uwekezaji mzuri,” anasema.
ZIPA imeboresha mchakato wa uidhinishaji wa uwekezaji na kutoa motisha kwa maendeleo rafiki kwa mazingira, miradi ya utalii ya jamii, na maeneo ya malazi ya kifahari yanayolingana na vipaumbele vya uhifadhi wa kisiwa hicho. SOMA: ATCL kuongeza vituo vitatu kimkakati
Kwa sasa, Vumawimbi bado haijaendelezwa kwa ipasavyo, lakini wawekezaji wameanza kuuliza kuhusu fursa zenye udhibiti za nyumba za kulala wageni zinazodumisha haiba ya asili ya eneo hilo. Uungwaji mkono na Serikali Katika ajenda yake ya utalii, Rais Mwinyi anaiweka Pemba si kama kivutio cha soko kubwa la fukwe, bali kitovu cha utalii wa mazingira mahali ambapo wageni wanatafuta ukweli wa utamaduni wa asili.



