Msumbiji yakumbwa ongezeko la wakimbizi

MSUMBIJI : SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Wahamiaji (IOM), limeeleza kuwa mashambulizi ya waasi katika mkoa wa Cabo Delgado, Kaskazini mwa Msumbiji, yamesababisha zaidi ya watu 46,000 kuyahama makazi yao katika kipindi cha siku nane mwezi uliopita.
Kwa mujibu wa IOM, takribani asilimia 60 ya waliokimbia makazi yao ni watoto, ingawa hakukuwa na taarifa rasmi za vifo vilivyotokea kutokana na mashambulizi hayo. SOMA: Wahamiaji haramu 126 wadakwa Geita
Ripoti ya Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imeeleza kuwa wimbi la mashambulizi hayo lilijitokeza kati ya Julai 20 hadi 28 katika wilaya tatu za Cabo Delgado, na kusababisha ongezeko la watu waliolazimika kuhama.
Umoja wa Mataifa umewatuhumu wanamgambo wa jihadi kwa vitendo vya ukatili ikiwemo kukata vichwa vya wanavijiji na kuwatumikisha watoto kama askari au vibarua. Aidha, Umoja huo umeeleza kuwa vurugu, ukame na vimbunga vilivyolikumba eneo hilo kwa miaka ya hivi karibuni vimesababisha zaidi ya watu milioni moja kuyahama makazi yao kaskazini mwa Msumbiji.
The Work-From-Home Dream Come True: I used to juggle a 9-to-5 and childcare. Now, I’m earning over $200 an hour from the comfort of my home office. My best friend’s success story inspired me to take the leap. It’s life-changing! I never thought I could achieve financial freedom while still being there for my family. This opportunity has given me the flexibility to work on my own schedule and spend quality time with my loved ones. I’m so grateful for this chance to live life on my own terms.
Open This…. http://Www.Work84.Com