Rais Samia aunda Tume Huru kuchunguza vurugu za uchaguzi
RAIS Samia Suluhu Hassan ameunda Tume Huru ya kufanya uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 29, 2025 na amemteua Jaji Mkuu mstaafu, Mohamed Chande Othmani kuwa Mwenyekiti wa tume hiyo.
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi na kusainiwa na Balozi Dk Moses Kusiluka ilisema Rais Samia amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo chini ya kifungu cha 3 cha Sheria Tume za Uchunguzi, Sura ya 32.
Sambamba na hayo, Rais Samia ameteua wajumbe wa tume hiyo ambao ni Jaji Mkuu mstaafu wa Mahakama ya Tanzania, Profesa Ibrahim Juma na Mwanadiplomasia na Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu, Balozi Ombeni Sefue.
Aidha, wajumbe wengine walioteuliwa katika tume hiyo ni pamoja na Mwanadiplomasia na Balozi mstaafu, Balozi Radhia Msuya, Mwanadiplomasia na Balozi mstaafu, Paul Meela na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) mstaafu, Said Mwema.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wajumbe wengine wa tume hiyo walioteuliwa na Rais Samia ni Mwanadiplomasia na Balozi mstaafu, Balozi David Kapya na aliyewahi kuwa Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Dk Stergomena Tax.
Hivi karibuni wakati akilifungua Bunge la 13, Rais Samia aliwaahidi Watanzania kuunda Tume ya Uchunguzi kuchunguza vurugu zilizojitokeza wakati na baada ya uchaguzi kwa lengo la kujua wahusika waliochochea vurugu hizo.
Alisema matokeo ya uchunguzi huo yatakuwa mwanzo wa kuanzisha mchakato wa mazungumzo na maridhiano ya kitaifa yatakayosaidia kuliunganisha taifa, hali itakayosaidia kudumisha amani na utulivu.
“Mimi binafsi, wabunge, nimehuzunishwa sana na tukio lile. Natoa pole kwa familia zote zilizopoteza wapendwa wao. Naomba Mwenyezi Mungu awapumzishe kwa amani na majeruhi tunawaombea wapone mapema. Na kwa wale waliopoteza mali zao, tunawaomba wawe na uvumilivu,” alisema rais.
Aliongeza: “Serikali imechukua hatua ya kuunda tume kuchunguza yaliyotokea ili tujue kiini cha tatizo na taarifa itakayotolewa na tume hiyo, itatuongoza katika mazungumzo ya kuleta amani na maelewano nchini.”




Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us →→→→→→→ https://Www.Work27.Online
I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
.
HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com