Samia aahidi ajira 5,000 siku 100 za kwanza

KOROGWE: Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuwa endapo atapewa ridhaa ya kuendelea kuiongoza nchi, ataanza kwa kuajiri watumishi 5,000 katika sekta ya afya ndani ya siku 100 za kwanza.
Watumishi hao watasambazwa katika vituo vya afya vinavyoendelea kujengwa nchi nzima.
Ahadi hiyo ameitoa leo, Septemba 30, 2025, wakati akihutubia maelfu ya wakazi wa Korogwe, mkoani Tanga, ikiwa ni sehemu ya kampeni zake kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu.
Akizungumzia suala la huduma ya afya, Dk. Samia amesema pia serikali yake itaendelea kuboresha huduma za bima ya afya ili kuhakikisha matatizo kama ya kushikiliwa kwa maiti hospitalini yanakomeshwa.
“Bima ya afya itakwenda kutuondolea lile tatizo la kishikilia maiti, mtu anapotangulia mbele za haki, malipo hayajalipwa, madaktari wanaoendesha hospitali wanazuia maiti mpaka malipo yalipwe, hivyo suluhu yake ni bima ya afya, kila mmoja wetu akiwa na bima ya afya, malipo yakilipwa kwa bima hakitakuwa na haja ya kuzuia miili iliyotangulia mbele ya haki” amesema Dk. Samia.
Akizungumzia kuhusu huduma ya maji, Dk. Samia ameeleza kuwa serikali imepiga hatua kubwa katika kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama, na kuongeza kuwa juhudi za kumtua mama ndoo kichwani zinaendelea.
“Tumeinua upatikanaji wa maji, tumefanikiwa kumtua mama ndoo kichwani lakini bado hatujamaliza kuwatua wamama wote kuwatua ndoo kichwani, lengo letu ni kila mtanzania awe na maji safi na salama karibu, kwahiyo hii kazi bado inaendelea” amesema Dk. Samia.
Dk. Samia aliwataka wananchi waendelee kuiamini CCM kwa kuwa imejipanga kuendeleza maendeleo yaliyokwisha kuanzishwa, hususan katika sekta muhimu kama afya na maji.
JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com