TMDA yajipanga mikakati mipya utekelezaji dira 2050

DAR ES SALAAM: MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imejadili rasimu ya mpango mkakati mpya wa mamlaka wa miaka mitano unaoakisi utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050.

Haya yalijiri wakati Menejimenti ya TMDA ilipokutana mkoani Morogoro Februari 2 hadi 3, 2026.

Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dk Adam Fimbo, aliwaeleza wajumbe wa kikao husika kuwa rasimu husika ya mpango mkakati inabeba Dira mpya ya TMDA ambayo ni kuimarika kwa afya na ustawi wa Watanzania wote kupitia udhibiti bora unaokidhi viwango vya kitaifa.

Dk Fimbo aliongeza kuwa  dhamira mpya ya taasisi itakuwa kulinda afya ya jamii kwa kuhakikisha, usalama, ubora na ufanisi wa dawa, vifaa tiba, vitendanishi na bidhaa zote zinazohusiana na afya”.

Amesema rasimu ya mpango mkakati huo ni ya sita kufuatia kukamilika kwa ufanisi kwa mpango mkakati wa tano. Mpango mkakati wa sita wa TMDA unatarajiwa kuanza kutumika Julai 01, 2026.

Pamoja na mambo mengine, rasimu ya mpango mkakati husika inalenga katika kuhakikisha ubora, usalama na ufanisi wa bidhaa za dawa, vifaa tiba na vitendanishi kwa lengo la kulinda afya ya jamii.

Uongozi wa TMDA imekuwa na utamaduni shirikishi katika kujadili mambo makubwa yahusuyo taasisi, ambapo watumishi wote hushirikishwa kupitia ngazi mbalimbali ndani ya mamlaka kabla ya kuidhinishwa na Bodi ya Ushauri ya Wizara kwa TMDA (MAB).

Mpango Mkakati huo mpya unaweka mwelekeo wa pamoja katika udhibiti, utasaidia katika kupanga matumizi ya rasilimali vizuri na kuboresha uwajibikaji na uwazi.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button