Watumishi watakiwa kufundwa sheria za kazi

ARUSHA: NAIBU Katibu Mkuu,Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Walemavu, Zuhura Yunus amewahimiza waajiri kote nchini kujenga utamaduni wa kuwajengea uwezo watumishi hususani mafunzo ya mara kwa mara na kuwakumbusha sheria na kanuni za kazi ili kuondoa migogoro katika maeneo kazi.

Zuhuru alisema hayo jana wakati akifungua semina ya waajiri serikalini na Viongozi wa Chama Cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania {TUGHE} alisema wajiri wote nchini wajenge utamaduni kwa watumishi wao katika kutoa mafunzo ya mara kwa mara lengo ni kuwajengea uwezo watumishi kujua wajibu wao kazini kwani kufanya hizo  itakuwa ni mwarobaini wa  kutibu na kuondoa migogoro.

Alisema watumishi pamoja na wajiri wakielewa vyema taratibu ,miongozo ,sheria na kanuni zinazosimamia utumishi wa umma  na masuala ya ajira  na mahusiano kazini  haitakuwa rahisi kuzikiuka.

Naibu Katibu Mkuu huyo aliendelea kusema kuwa waliopata fursa ya mafunzo hayo watakaporejea maeneo ya kazi wahakikishe wanapata wasaa wa kuwajuza wengine yale aliyojifunza ili wote wapate kuwa na uelewa wa kutosha katika nmajukumu yao ya kazi.

“Serikali yetu  inayoongozwa na Dk.Samia Suluhu Hassan  imekuwa mstari wa mbele  kushughulikia na  kuzipatia ufumbuzi  changamoto mbalimbali  za watumishi na kero zilizokuwa ni kikwazo  zimepatiwaa utauzi”,aliongeza Yunus.

Katibu Mkuu wa TUGHE, Hery Mkunda alisema kuwa semina hiyo ya siku tano inashirikisha washiriki zaidi ya washiriki 800 alisema semina hiyo inalenga kujengeana uwezo,kubadilishana uzoefu  na kujenga uhusiano chanya  baina ya washiriki kukumbusha haki na wajibu wa mfanyakazi na maadili sehemu za kazi pia kuhamasisha ushirikishwaji.

“Mafunzo hayo  yalianza mwaka 2018 ambapo jumla ya viongozi wa matawi na waajiri wapatao 4713 wamepata mafunzo kupitia semina hizo idadi ya washiriki imekuwa ikiongezeka kila mwaka na matunda yake yamesaidia kupunguza migogoro baina ya watumishi na waajiri,”alisema Mkunda.

Mkunda alisema TUGHE wanaipongeza serikali kwa namna ambavyo im ekuwa ikishughulikia changamoto mbalimbali za wafanyakazi na kusema wote ni mashahidi hoja nyingi zilizokuwa zikitukabili wafanyakazi zimepatiwa ufumbuzi na kuongeza ari na uwajibikaji wa wafanyakazi hapa nchini.

Mfano wa mambo machache moja ni ya hili la hivi karibuni ambalo ni nyongeza ya siku za likizo kwa wafanyakazi wanawake wanaojifungua watoto njiti  sambamba na kuingiza  mbadiliko haya kwenye sheria ya ajira na mahusiano kazini na suala hili lilianzia Baraza la wafanyakzi la TUGHE.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button