Wazee Dar wapinga uchochezi uchaguzi mkuu

DAR ES SALAAM: WAZEE wa jiji la Dar es Salaam wanapinga kauli za kuhamasisha wananchi kususia uchaguzi, wakisisitiza kuwa maneno hayo hayana tija na yanahatarisha mshikamano wa taifa.
Mkurugenzi wa Shirika la Vijana na Wanawake (TAFEYOCO), Elvis Makumbo, amsema kuna watu wanaojificha kwenye mwamvuli wa uzalendo lakini ajenda yao ni kutafuta viongozi watakaowapa manufaa binafsi.
“Tusifate maneno ya wenye uchu wa madaraka. Tulipata uhuru kwa njia ya amani, basi tuwachague viongozi kwa amani kwa kufuata utaratibu wa nchi,” amesema.
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Ushauri Mtaa wa Jogoo, Romald Rwechungura, anasisitiza kuwa wazee hawawezi kukaa kimya mbele ya wito wa kususia uchaguzi. “Wazee tukinyamaza ni sawa na kuridhia jambo lisilofaa. Tunataka vijana wetu washiriki na kuimarisha demokrasia,” amesema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Kata ya Goba, Yahaya Mjema, anakumbusha kuwa amani ni urithi uliotengenezwa tangu enzi za uhuru.
“Hatuna tofauti ya dini wala kabila. Tunaliomba Jeshi la Polisi liwe na hekima na subira kukabiliana na changamoto za uvunjifu wa amani,” amesema. Katibu wa Kikundi cha Uwazi kilichopo Mbezi Luis, Ahmad Tamla, anaongeza kuwa wazee wanapaswa kupewa nafasi zaidi kwenye ngazi za maamuzi.
“Elimu ya siasa iliyokuwa inafundisha uzalendo irudi. Uchaguzi utafanyika, na sisi wazee tunasisitiza tutii mamlaka ya nchi kwa mujibu wa katiba na sheria,” amesema.
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com
JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com