Zahanati kupunguza vifo vya wajawazito

KIGOMA: KUKAMILIKA kwa Zahanati ya Lemba iliyopo Kijiji cha Kasumo Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma kutapunguza vifo vya wajawazito wakati wa kujifungua kutokana na hapo awali kufuata huduma za afya umbali mrefu.
Mkuu wa Wilaya Buhigwe, Michael Ngayarina amesema hayo akitoa maelezo ya utekelezaji wa mradi kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Ismail Alli Ussi wakati ukianza mbio zake wilayani Buhigwe kutembelea miradi mbalimbali.
Ngayarina amesema kuwa kabla kujengwa kwa zahanati hiyo wananchi walikuwa wakitembea kilometa nane kuelekea kijiji cha Muyama katika wilaya hiyo ya Buhigwe kufuata huduma hiyo ya matibabu au kutembea kilometa 18 kwenda kupata huduma katika Kituo cha Afya Shunga Wilaya ya Kasulu jambo ambalo lilikuwa usumbufu mkubwa.
Kutokana na changamoto hiyo mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa wananchi walianza kuchangishana wenyewe ili kuanza kutekeleza mradi huo ndiyo serikali kuu, Halmashauri na wadau mbalimbali wakawaunga mkono na kukamilisha mradi huo hadi kuanza kutoa huduma ambapo milioni 130 zimetumika hadi kukamilika.
Akizungumza katika uzinduzi wa mradi huo Kiongozi wa Mbio za Mwenge Uhuru, Ismail Alli Ussi aliwapongeza wananchi wa kijiji hicho na kusema kuwa moyo wa kizalendo ndiyo uliowasukuma kufanya hivyo na kuwataka kuendelea kujitolea kwa hali na mali katika kushiriki kwenye shughuli za maendeleo.
Ussi amesema kuwa pamoja na jitihada hizo serikali imeendelea kutekeleza kwa kuanzisha miradi mipya ya maendeleo inayogusa maisha ya wananchi lakini pia kumalizia miradi ikiwemo ya utoaji huduma iliyoanzishwa na wananchi ukiwemo mradi huo wa Zahanti ya Lemba wilayani Buhigwe.
YALIYOJIFICHA MOCHWARI, HATOSAHAU, MAITI KUFUFUKA, KUPAKWA MAKEUP ALIEKAA MIAKA 7 ANAHUDUMIA MAITI
542,245 views · 4 years ago…more
YALIYOJIFICHA MOCHWARI, HATOSAHAU, MAITI KUFUFUKA, KUPAKWA MAKEUP ALIEKAA MIAKA 7 ANAHUDUMIA MAITI
542,245 views · 4 years ago…more
MSHTUKO: MAITI YAKUTWA IKIELEA KWENYE DIMBWI LA MAJI MOROGORO, ZIMAMOTO WAINGIA KUITOA…
MAITI YAKUTWA IMEFUKIWA KWENYE NYUMBA YA MTU TABORA YADAIWA ALITEKWA
MSHTUKO! MAITI YAKUTWA IKIELEA MTONI, ALIYESHUHUDIA MWILI AFUNGUKA – ”INAONEKANA AMENYONGWA”…
MIILI ZAIDI YA 200 KUFUKULIWA VINGUNGUTI, MEYA AFUNGUKA “MIILI MINGI IMESOMBWA NA MAJI “