Mchinjita kuanza ziara Kilimanjaro, Tanga, Dar

DAR ES SALAAM: Makamu Mwenyekiti Bara wa Chama cha ACT Wazalendo, Isihaka Mchinjita atakuwa na ziara ya siku saba kwenye majimbo ya mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Kilimanjaro kuanzia Januari 10, hadi 16, 2026.
–
Kwenye ziara hiyo ya kwanza tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu 2025, Mchinjita atakutana na viongozi wa chama hicho wa mikoa na majimbo pamoja na waliokuwa wagombea wa ubunge na udiwani kwa ajili ya kusikiliza maoni yao na kufafanua misimamo mbalimbali iliyochukuliwa na chama baada ya uchaguzi huo.
–



