Manispaa Geita yawahakikishia usalama wahitaji shuleni

HALMASHAURI ya Manispaa ya Geita imeweka wazi kuwa imejipanga kikamilifu kuhakikisha kila shule inakuwa na miundombinu rafiki kwa watoto ambao ni wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Rashid Muhaya ameeleza hayo katika hafla ya kupokea msaada viti mwendo, vifaa vya kujifunzia na michezo kutoka kampuni ya Isamilo.
Amesema ili kuweka mazingira rafiki ya kujifunzia kwa makundi maalum halmashauri imesimamia kuhakikisha ujenzi wa miundombinu inayotoa mwanya rahisi kwa watoto hao kujifunza.

Amesema kwa kufuata muongozo wa elimu kila shule imejengewa vyoo na madarasa yenye miundombinu inayomwezesha mtoto mwenye mahitaji maalum kuingia na kutoka kwa urafiki.
Muhaya amekiri kuwa mbali na juhudi hizo bado kuna uhitaji wa vitabu vya watoto hususani kundi hilo maalum hvivo wadau wote wa maendeleo wanaombwa kuguswa kuwasaidia watoto hao.
“Tunatoa wito kwa wazazi wote pamoja na watoa taaluma kwamba watoto hawa wenye mahitaji maalum basi waingie shuleni ili wanufaike na haki yao moja kwa moja,” amesema.
Meneja wa Isamilo, Robison Mageta amesema msaada huo wa kundi maalum una thamani ya sh milioni tano ni sehemu ya Uwajibikaji wa Kampuni kwa Jamii (CSR).

Amesema CSR yao kwa mwisho wa mwaka 2025 imegusa zaidi kundi hilo lenye uhitaji mkubwa kwa kuwapa vifaa vitakavyowasaidia kukidhi mahitaji ya msingi kwenye sekta ya afya na elimu.
Mageta ametaja baadhi ya misaada waliyotoa ni pamoja na viti mwendo, vitabu na vifaa vya kutembelea pamoja na vitu vingine muhimu.
“Tunaomba pia wakandarasi wengine wenye makampuni kuendelea kushirikiana na serikali katika kufanikisha huduma bora kwa jamii hususani ya watu wenye mahitaji maalum,” amesema.




I make up to $220 an hour working from my home. My story is that I quit working at Walmart to work online and with a little effort I easily bring in around $450h to $890h… Someone was good to me by sharing this link with me, so now I am hoping I could help someone else out there by sharing this link.Try it, you won’t regret it!.
HERE→→→→→→→→→→ https://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com