Dk Nchimbi ahadharisha kutonesha vidonda vya vurugu za Oktoba 29
MAKAMU wa Rais, Balozi Dk Emmanuel Nchimbi amesema si vyema kwa viongozi wa serikali, asasi za kijamii, viongozi wa vyama vya siasa na wanaharakati kuzungumzia yaliyojiri Oktoba 29, mwaka jana nje ya mfumo wa kisheria.
Dk Nchimbi alisema hayo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria na kuzinduliwa kwa mwaka mpya wa shughuli za kimahakama kwa mwaka 2026 Dodoma.
Alisema Rais Samia Suluhu Hassan ameshaunda Tume ya Kuchunguza Matukio Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu 2025 ili kushughulikia suala hilo.
“Namshukuru Rais wa TLS ametuasa viongozi, kuwa si vizuri kuendelea kuzungumzia yaliyojiri Oktoba 29 kwa sababu yanatonesha vidonda na pengine yanaweza yasisaidie sana katika mchakato wa haki, kwanza nakubaliana naye kwa asilimia 100,” alisema Dk Nchimbi.
Aliongeza: “Niongeze pale aliposahau, kwamba si viongozi wa serikali pekee na viongozi wa vyama vya siasa, taasisi za kijamii na wanaharakati. Rais (Samia) ameunda Tume inaendelea kufanya kazi, kuendelea kuzungumza nje ya mfumo wa kisheria uliowekwa kwa jambo hili ni kutolitendea haki taifa letu”.
Dk Nchimbi alisema ni muhimu kwa kila mtu anayeipenda Tanzania akubaliane na Rais wa TLS watu wasitoneshane na watoe nafasi kwa vyombo vya kisheria kutimiza wajibu wake.
Pia, aliipongeza TLS kwa kutoa mchango mkubwa na kwa kushirikiana kikamilifu na Serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na taasisi nyingine katika utoaji wa huduma za msaada wa kisheria kwa wananchi wasio na uwezo wa kumudu gharama za uwakili.
“Napenda kuwahakikishia kuwa serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa TLS na wadau wengine wote wa
haki ili kufikisha huduma za kisheria kwa wananchi kwa wakati na kwa ufanisi,” alisema.




this is one of the best article i read today, i enjoy reading how you structure this article, keep up the good work, my site is the best webdesign freelancer in berlin in Germany, https://webdesignfreelancerberlin.de/ you can check it out. Thank you
Good article. I will be going through a few of these issues as well..