Ulinzi upo imara Mwanza

MWANZA: MKUU wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda amepongeza Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza Kwa kuimarisha ulinzi na usalama.
Mtanda alisema hayo Mei 9 katika maadhimisho ya Siku ya Familia ya Jeshi la Polisi yaliyofanyika katika uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.
Mtanda amesema Jeshi la Polisi mkoani humo linaendelea kuhakikisha amani, utulivu na usalama unaimarika.

Amesema kuwa kazi inayofanywa na askari wa jeshi hilo imekuwa chachu ya maendeleo kutokana na wananchi kuendelea kufanya shughuli zao za kiuchumi katika mazingira salama na yenye utulivu.
Amesema serikali inatambua mchango mkubwa wa Jeshi la Polisi katika kulinda raia na mali zao, huku akiwasisitiza askari kuendelea kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na uzalendo mkubwa kwa taifa.
“Jeshi la Polisi limeendelea kufanya kazi nzuri ya kuimarisha ulinzi na usalama. Serikali inatambua na kuthamini juhudi zinazofanywa na askari wetu katika kuhakikisha wananchi wanaishi kwa amani na usalama wakati wote,” amesema Mtanda.
Amesema serikali ya awamu ya sita imeendelea kuboresha mazingira ya kazi kwa askari polisi nchini kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa vituo vya polisi, nyumba za askari pamoja na kuongeza vitendea kazi vya kisasa.




Google pays $95 on a regular basis. My latest salary check was $8200 for working 10 hours a week on the internet. My younger sibling has been averaging $15k for the last few months, and he constantly works approximately 24 hours. I’m not sure how simple it was once I checked it out. This is my main concern… GOOD LUCK…. http://www.giftpay7.vip